RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amekutana na Brigedia Jenerali Fadhil Omar Nondo aliyefika Ikulu mjini Zanzibar kwa ajili ya kujitambulisha baada ya kuteuliwa kuwa Mkuu mpya wa  Brigedi ya Nyuki Zanzibar. 
Dk. Shein alitumia fursa hiyo kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli ambaye pia, ni Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi kwa kumteua Brigedia Jenerali Fadhil Omar Nondo kushika wadhifa na kumpongeza Brigedia huyo huku akimuhakikishi kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar chini ya uongozi wake itampa mashirikiano makubwa kama ilivyofanya kwa viongozi waliokuwepo kabla yake. 
Nae, Brigedia Jenerali Nondo alimuahidi Dk. Shein kuwa ataendeleza uhusiano na ushirikiano mwema ulipo kati ya Majeshi ya Ulinzi Tanznia  pamoja na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar huku akisifu mashirikiano mazuri anayoyapata kutoka kwa viongozi wa Serikali na viongozi wa vikosi vya ulinzi vya SMZ na kuahidi kutoa ushirikiano kwao pamoja na kwa wananchi wote wa Zanzibar. 
Brigedia Jenerali Fadhil Omar Nondo anashika nafasi ya Marehemu Bregedia Jenerali Cyril Ivor Mhaiki, aliyekuwa Kamanda wa Brigedia ya Nyuki Zanzibar, ambaye alifariki dunia tarehe 13, Disemba mwaka 2016 huko katika Hospitali ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania, Lugalo jijini Dar-es-Salaam na kuzikwa Mkoani kwao Ruvuma. 
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na Brigedia Jenerali Fadhil Omar Nondo alipofika kujitambulisha leo Ikulu Mjini Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiagana na  Brigedia Jenerali Fadhil Omar Nondo baada ya mazungumzo alipofika kujitambulisha leo Ikulu Mjini Zanzibar
 (Picha na Ikulu)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...