Mkuu wa mkoa wa Arusha Mhe Mrisho Gambo akikaribishwa na Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa Mhe. Samwel Shelukindo katika ubalozi wetu uliopo jijini Paris. Mhe Gambo yupo katika ziara ya mafunzo nchini Ufaransa, ambapo pamoja na mafunzo hayo amekua akiutangaza mkoa wa Arusha kama kitovu cha utalii nchini Tanzania. 

Mhe Gambo, akiwa huko mefanya mazungumzo na Balozi Shelukindo, na kubadilishana mawazo ya namna ya kuvutia wananchi wa nchi hiyo kutembelea Tanzania. 

Ufaransa ni moja ya zinazoleta watalii wengi nchini Tanzania. Pamoja na mambo mengine  Mhe RC na Balozi wamejadiliana mambo ya Msingi ya kufanya ili kuongeza watalii kutoka Ufaransa kuja Arusha, kupata wawekezaji kutoka Ufaransa kuja Arusha pamoja na namna ya kutangaza fursa za uwekezaji zilizopo Mkoani humo, pamoja na kuanzisha tukio la kimataifa la kutangaza utalii mkoani Arusha kila mwaka.
Mkuu wa mkoa wa Arusha Mhe Mrisho Gambo akiweka saini katika kitabu cha wageni baada ya kukaribishwa na Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa Mhe. Samwel Shelukindo katika ubalozi wetu uliopo jijini Paris. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...