Ubalozi wa Kuwait nchini kwa kushirikiana na Taasisi  ya Human Relief wamekabidhi msaada wa vyakula mbalimbali kwa Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema kwa ajili ya watu wasiojiweza na mayatima ili kupata futari katika mwezi huu Mtukufu wa Ramadhani.

Akizungumza baada ya kupokea msaada huo mapema leo, Mjema amesema, chakula hicho kitapelekwa katika vituo vya watoto yatima na wasiojiweza ili waweze kuufurahia mwezi wa Ramadhani.

"Chakula hiki tunaenda kuwapa wananchi ambao hawana uwezo na familia ambazo kwa kweli tunaona hwana uwezo," alisema Mh. Mjema.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa kampuni ya Bigbon, Mohammed Bahashwan amesema, taasisi hiyo imekuwa ikitoa misaada mbalimbali na hasa kwa mayatima bila kujadili dini zao,amesema na kuongeza kuwa kuwa mbali na kutoa misaada hiyo lakini pia taasisi hiyo imekuwa ikijenga visima na misikiti katika maeneo mbalimbali nchini.

Kwa upande wake, balozi wa Kuwait nchini, Mhe Jaseem Al Najem amesema kuwa, nchi hiyo itaendelea kushirikiana na serikali katika mambo mbalimbali ya kusaidia jamii.

Amesema msaada huo wameanza na wilaya ya Ilala lakini watakuwa wakitoa misaada na maeneo mengine kulinga na uhitaji wa mambo mbalimbali katika jamii nzima kwa kushirikiana na serikali.

Mkuu wa Wilaya ya Ilala ,Sophia Mjema (kulia) akipokea Msaada wa vyakula mbalimbali kutoka kwa Balozi wa Kuwait nchini Mhe. Jaseem Al Najem.Pichani kushoto ni Katibu Tawala wilaya ya Ilala,Edward Mpogolo.

Mkuu wa Wilaya ya Ilala ,Sophia Mjema Akizungumza wa Globu ya jamii baada ya kupokea msaada huo.
Mkuu wa Wilaya ya Ilala ,Sophia Mjema na Balozi wa Kuwait nchini Mhe. Jaseem Al Najem wakiwa katika picha ya pamoja. leo Jijini Dar es Salaam.Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii.
Balozi wa Kuwait nchini Tanzania Mhe. Jaseem Al Najem akiwasili katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ilala ,Sophia Mjema.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...