Ubalozi
wa Kuwait nchini kwa kushirikiana na Taasisi ya Human Relief
wamekabidhi msaada wa vyakula mbalimbali kwa Mkuu wa Wilaya ya Ilala,
Sophia Mjema kwa ajili ya watu wasiojiweza na mayatima ili kupata futari
katika mwezi huu Mtukufu wa Ramadhani.
Akizungumza
baada ya kupokea msaada huo mapema leo, Mjema amesema, chakula hicho
kitapelekwa katika vituo vya watoto yatima na wasiojiweza ili waweze
kuufurahia mwezi wa Ramadhani.
"Chakula hiki tunaenda kuwapa wananchi ambao hawana uwezo na familia ambazo kwa kweli tunaona hwana uwezo," alisema Mh. Mjema.
Kwa
upande wake, Mkurugenzi wa kampuni ya Bigbon, Mohammed Bahashwan
amesema, taasisi hiyo imekuwa ikitoa misaada mbalimbali na hasa kwa
mayatima bila kujadili dini zao,amesema na kuongeza kuwa kuwa mbali na kutoa misaada hiyo lakini pia taasisi hiyo imekuwa ikijenga visima na misikiti katika maeneo mbalimbali nchini.
Kwa
upande wake, balozi wa Kuwait nchini, Mhe Jaseem Al Najem amesema kuwa,
nchi hiyo itaendelea kushirikiana na serikali katika mambo mbalimbali
ya kusaidia jamii.
Amesema
msaada huo wameanza na wilaya ya Ilala lakini watakuwa wakitoa misaada
na maeneo mengine kulinga na uhitaji wa mambo mbalimbali katika jamii
nzima kwa kushirikiana na serikali.
Mkuu wa Wilaya ya Ilala ,Sophia Mjema (kulia) akipokea Msaada wa vyakula mbalimbali kutoka kwa Balozi wa Kuwait nchini Mhe. Jaseem Al Najem.Pichani kushoto ni Katibu Tawala wilaya ya Ilala,Edward Mpogolo.
Mkuu wa Wilaya ya Ilala ,Sophia Mjema Akizungumza wa Globu ya jamii baada ya kupokea msaada huo.
Mkuu wa Wilaya ya Ilala ,Sophia Mjema na Balozi wa Kuwait nchini Mhe. Jaseem Al Najem wakiwa katika picha ya pamoja. leo Jijini Dar es Salaam.Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii.
Balozi wa Kuwait nchini Tanzania Mhe. Jaseem Al Najem akiwasili katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ilala ,Sophia Mjema.
Mkuu wa Wilaya ya Ilala ,Sophia Mjema (kulia) akipokea Msaada wa vyakula mbalimbali kutoka kwa Balozi wa Kuwait nchini Mhe. Jaseem Al Najem.Pichani kushoto ni Katibu Tawala wilaya ya Ilala,Edward Mpogolo.
Mkuu wa Wilaya ya Ilala ,Sophia Mjema Akizungumza wa Globu ya jamii baada ya kupokea msaada huo.
Mkuu wa Wilaya ya Ilala ,Sophia Mjema na Balozi wa Kuwait nchini Mhe. Jaseem Al Najem wakiwa katika picha ya pamoja. leo Jijini Dar es Salaam.Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii.
Balozi wa Kuwait nchini Tanzania Mhe. Jaseem Al Najem akiwasili katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ilala ,Sophia Mjema.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...