Muft
Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeir amewataka watanzania na waislamu kwa
ujumla kupendeza kwa kuvaa mavazi yanayotengenezwa na kampuni ya mzawa Mussa
Bakari ya 'Islamic Fashion Tanzania'.
Kiongozi huyo waislamu nchini ametoa kauli hiyo Jijini Dar es Salaam
Jumapili wakati akizindua kampuni hiyo ya mavazi ya kiislamu na kueleza kuwa
kwa mujibu wa maandiko ya dini hiyo, wameamrishwa kupendeza kwani Mungu ni
mzuri na na hupenda vitu vizuri.
Mufti alifafanua kuwa uislamu huambatana na
usafi na usafi huo unaanzia kwenye mavazi, hivyo ni vyema waislamu wakaitumia
fursa hiyo kwa kununua mavazi kutoka kwenye kampuni hiyo ya mzawa.
Pia
ameishauri kampuni hiyo kujitangaza zaidi kwani hitaji wa vazi hilo ni mkubwa
nchi nzima na sio tu kwa mkoa wa Dar es Salaam, na akawaomba watume muwakilishi
kwenye sherehe za Eid El Fitr zinazotaraji kufanyika Mkoani Kilimanjaro
kitaifa, ili wakazitangaze bidhaa zao na huko.
"Ni vyema pia waislamu
wakaambizana habari njema za ujio wa Islamic Fashion Tanzania ili wengi waweze
kunufaika kwa kupendeza na mavazi yao" alisema Mufti Mkuu.
Kwa upande wake
Mkurugenzi wa Kampuni hiyo ya Islamic Fashion Tanzania Mussa Bakari ameeleza
kuwa kampuni hiyo imeanza tangu mwaka 2014 ambapo walikuwa wanategemea mavazi
hayo kutoka nchi za nje, kutokana na kwa jitihada walizofanya \ sasa wameweza
kutengeneza mavazi yao ambapo nusu ya uzalishaji inafanyika Dubai na
kumalizikia Tanzania.
Mkurugenzi Mussa Bakari ameongeza kuwa changamoto ya
Watanzania kukosa kanzu zenye ubora kwa muda mrefu ndiyo zimewapelekea wao
kuanzisha Islamic Fashion Tanzania, ili kuwarahisishia watanzania waliokuwa
wanasafiri kwenda nje ya nchi wapate kanzu zenye ubora. Hivyo amewaomba
watanzania kumuunga mkono ili aweze kupiga hatua zaidi za kuwahudumia
watanzania.
Muft Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeir (kulia) akizungumza jijiini Dar es Salaamn wakati uzindui wa mavazi yanayotengenezwa na kampuni ya mzawa Mussa Bakari ya 'Islamic Fashion Tanzania.
Mkurugenzi wa Kampuni hiyo ya Islamic Fashion Tanzania Bw. Mussa Bakari akiwaomba watanzania kumuunga mkono ili aweze kupiga hatua katika uzindui huo.
Muft Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeir (kulia) akizindua mavazi yanayotengenezwa na kampuni ya mzawa Mussa Bakari ya 'slamic Fashion Tanzania kwa kushirikiana Shehe mkuu wa mkoa wa Dar es salaam,Sheikh Alhad Mussa Salim (katikati) na Mkurugenzi wa Kampuni hiyo Bw. Mussa Bakari.
Sehemu ya viongozi na wageni mbalimbali wakiwa katika uzinduzi huo.
Sehemu ya viongozi na wageni mbalimbali wakiwa katika uzinduzi huo.Picha na Emmanuel Maasaka,Globu ya Jamii.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...