Waziri wa Mambo ya Ndani na Mbunge wa jimbo la Iramba Mkoani Singida Mwingulu L. Nchemba, amekabidhi gari la kubebea wagonjwa mpya na la kisasa ambalo limetolewa na serikali kupitia Wizara ya Afya, Jinsia, Wazee na Watoto kwa kituo cha afya cha Ndago kilichopo Wilayani Iramba.

Mwigulu ameagiza gari hilo lisitumike kama taksi au gari la kubebea mkaa, bali litumike kwa kazi iliyokusudiwa ambayo ni kubebea wagonjwa na akina mama wajawazito tu.

Mbunge huyo ameyasema hayo juzi wakati akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi ‘ambulance’ hiyo iliyofanyika katika kijiji cha Ndago jimbo la Iramba na kuhudhuriwa na mamia ya wananchi.

Aidha, amesema ni marufuku wagonjwa kuombwa kuchangia mafuta ya ambulance hiyo au gharama yo yote ile, gari hili wagonjwa walitumie bure.

“Gari hilo lipatikane kituoni wakati wote. Liwe na mafuta ya kutosha na dereva awepo. Gari hili ambalo ni la kisasa, litunzwe na kulindwa ili liweze kutumika kwa miaka mingi ijayo”, alisema Mwigulu.

Mbunge huyo ameishukuru serikali ya awamu ya tano chini ya rais Magufuli na waziri Ummy kwa msaada huo ambao utaokoa wapiga kura wake na wananchi kwa ujumla.

Awali mganga mfawidhi wa kituo cha afya cha Ndago, Dkt Lyoce Mgelwa, alisema kituo hicho kinahudumia tarafa nzima ya Ndago yenye wakazi 89,882.

Waziri wa Mambo ya ndani na Mbunge wa jimbo la Iramba Mkoani Singida Mwigulu Nchemba akiwasha gari la kubebea wagonjwa (ambulance), katika kijiji cha Urughu tarafa ya Ndago jimbo la Iramba.
Waziri wa Mambo ya ndani na Mbunge wa jimbo la Iramba mkoani Singida Mwigulu Nchemba akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi gari la kubebea wagonjwa (ambulance) katika kijiji cha Urughu tarafa ya Ndago jimbo la Iramba.
Mkazi wa kijiji cha Urughu jimbo la Iramba mkoani Singida Jumanne Hatibu akizungumza kwenye hafla ya makabidhiano ya gari la kubebea wagonjwa lililotolewa na serikali kupitia wizara ya afya jinsia, wazee na watoto.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...