Halila
Tongolanga amefariki jana usiku katika hospitali ya Muhimbili. Alikuwa
mwanamuziki wa siku nyingi na alifahamika kwanza kwa wengi baada ya
kuanza kusikika kibao chake cha lugha ya Kimakonde cha Kila munu ave na
kwao, chenye tafsiri ya ‘Kila mtu ana kwao’ ambacho alikirekodi akiwa
bendi ya jeshi ya CTU Monduli, iliyojulikana kama Les Mwenge.
Kwa
kifupi ni kuwa baada ya hapo aliitwa kujiunga na bendi iliyokuwa mali
ya Dr Alex Khalid, iliyokuwa ikiitwa Makondeko Six. Wakati huo Dr Khalid
alikuwa na sehemu kubwa ya burudani iliyokuwa pia na ukumbi na ilikuwa
inaitwa Makondeko ikawa na bendi ya watu sita hivyo bendi hiyo ikaitwa
Makondeko Six.
Bendi
hii awali ilikuwa ikipiga muziki kwa kufuata nyayo za bendi ya Tatu
Nane, lakini Dr Khalid baada ya kuona bendi haina umaarufu kutokana na
aina ya muziki iliyokuwa ikipiga, ndipo alipomuita Halila Tongolanga nae
akaja na baadhi ya wanamuziki wakajiunga na kuanzisha kundi
lililoendelea kutumia jina la Makondeko Six japo wanamuziki walikuwa
wengi zaidi ya sita.
Na
ndipo katika kundi hili lilikuwa na wanamuziki wengine kama Innocent
Nganyagwa, Anna mwaole wakaweza kurekodi tena wimbo wa Kila Munu Ave na
kwao na kundi kupata umaarufu mkubwa mpaka baada ya kusambaratika kwa
Makondeko baada ya kifo cha Dr Alex Khalid, lakini Tongolanga aliendelea
kutumia jina la Makondeko.
Tongolanga amefanya kazi nyingi za muziki ikiwemo kuwa mmoja wa kundi lililoundwa na wanamuziki wengine mahiri kama Moshi William, Muhidin Mwalim, Huluka Uvuruge, Kandaya na wengine lililojulikana kama Bana mwambe, ambapo waliweza kutoka nyimbo nyingi nzuri sana wakati biashara ya kuuza album ilipokuwa ina faida.
Balozi wa Msumbiji Bi Monica Patricio Clemente akiaga sanduku lililokuwa na mwili wa Halila Tongolanga
Baadhi ya wanamuziki waliowahi kufanya kazi na Tongolanga katika kundi la makondeko Six, wakiwa wanasubiri kusafirisha mwili wa mpendwa wao.Toka kushoto, Innocent Nganyagwa, Meneja wa bendi, mpiga solo, Waninga
John Kitime, wanamuziki wa Makondeko Six, Mngereza, Kumburu
Toka kushoto Rais wa Shirikisho la Sanaa za Ufundi Nyangamale, Balozi wa Msumbiji nchini, Katibu Mtendaji wa BASATA, Mbunge wa Tandahimba Mhe Katani Katani, afisa wa Ubalozi wa Msumbiji ,Tongolanga anategemewa kuzikwa kijijini kwao Mchichila kesho Junanne 6 Juni 2017.
Mungu Amlaze Pema Halila Tongolanga .
Baadhi ya wanamuziki waliowahi kufanya kazi na Tongolanga katika kundi la makondeko Six, wakiwa wanasubiri kusafirisha mwili wa mpendwa wao.Toka kushoto, Innocent Nganyagwa, Meneja wa bendi, mpiga solo, Waninga
John Kitime, wanamuziki wa Makondeko Six, Mngereza, Kumburu
Toka kushoto Rais wa Shirikisho la Sanaa za Ufundi Nyangamale, Balozi wa Msumbiji nchini, Katibu Mtendaji wa BASATA, Mbunge wa Tandahimba Mhe Katani Katani, afisa wa Ubalozi wa Msumbiji ,Tongolanga anategemewa kuzikwa kijijini kwao Mchichila kesho Junanne 6 Juni 2017.
Mungu Amlaze Pema Halila Tongolanga .
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...