Rais wa Shirikisho la Soka nchini (TFF), Jamal Malinzi na Katibu Mkuu wake, Celestine Mwesigwa wamepandishwa kizimbani leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es salaam na kusomewa mashtaka yanayo wakabili likiwemo la Kughushi waraka wa kamati ya utendaji ulioonyesha kuwa EXCOM imeridhia kubadilishwa kwa saini ya Bank, Kufanya fojari ya risiti za kuwa Malinzi anaidai TFF (risiti zipo zaidi 20 zinazodaiwa kufojiwa) hii inamhusu Malinzi pekee Na Mwisho ni shtaka la kutakatisha fedha dola za kimarekani zaidi ya laki tatu (hii inawahusu wote watatu ambao ni Malinzi, Mwesigwa na Nsiana). Watuhumiwa hao wamerudishwa rumande na kesi yao imepangwa kusikilizwa tena Julai 3, 2017.  Taarifa kamili itawajia baadae kidogo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Pole sana Ndg Malinzi na wenzako! Do ni shida kweli kweli!!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...