Mkuu wa Kitengo cha Wateja Wadogo na wa Kati wa Banki ya NMB, Omary
Mtiga akizungumza na zaidi ya watoto 450 waliopo kwenye mfungo mtukufu
wa Ramadhani kutoka vituo mbalimbali vya watoto yatima vya jijini Dar es
Salaam. NMB kwa kushirikiana na Mbunifu wa Mavazi nchini, Khadija
Mwanamboka ambaye ni mmiliki wa mgahawa wa VVK na wadau wengine katika
kuadhimisha Siku ya Mtoto wa Afrika wamefanikiwa kufuturisha watoto hao
yatima kutoka vituo mbalimbali vya jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Kitengo cha Wateja Wadogo na wa Kati wa Banki ya NMB, Omary
Mtiga (wa pili kulia) akitoa zawadi kwa watoto walioshiriki katika
futari iliyoandaliwa na Mbunifu wa Mavazi nchini, Khadija Mwanamboka
ambaye ni mmiliki wa mgahawa wa VVK na wadau wengine ikiwemo Benki ya
NMB katika maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika. Shughuli hiyo
ilifanyika katika ukumbi wa Shabaan Robert uliopo Upanga na kuhudhuriwa
na wageni mbalimbali pamoja na wadau waliosaidia kufanikisha jambo hilo
wakiwemo NMB na wengine.
Baadhi ya watoto waliopo kwenye mfungo mtukufu wa Ramadhani kutoka
vituo mbalimbali vya watoto yatima vya jijini Dar es Salaam wakiwa
katika futari iliyoandaliwa na NMB kwa kushirikiana na Mbunifu wa Mavazi
nchini, Khadija Mwanamboka ambaye ni mmiliki wa mgahawa wa VVK na wadau
wengine katika kuadhimisha Siku ya Mtoto wa Afrika.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...