Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Bw. Gerson Mdemu akitoa maelezo wakati wa Mkutano wa Kazi kati ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Wadau ( hawapo pichani)kutoka Taasisi mbalimbali za Serikali zilizopo Mkoani Tabora ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma. Madhumuni ya Kikao kazi hicho ilikuwa ni kukutana wa wadau hao kwa lengo la kujadiliana, kubadilishana mawazo na kuzitafutia ufumbuzi changamoto mbalimbali ambazo wadau hao pamoja na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wanakumbana nazo wakati wa utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku. Wadau walioshiriki kikao hicho ni kutoka Mahakama, Takukuru, Magereza, Polisi, Wakala wa Barabara, Maliasili, Halmashauri, Mawakili wa Serikali, Wanasheria na wanajamii. Kushoto kwa Naibu Mwanasheria Mkuu Wakili Mfawidhierikali Kanda ya Tabora Bw. Jackson Bulashi na kulia ni Kamanda wa Takukuru Tabora Bw. Fidelis Kalungura.
Sehemu ya wadau ambao wamekuwa na mazungumzo na majadiliano na Ujumbe wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ulioongozwa na Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Bw. Gerson Mdemu. Majadiliano hayo yamefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Takukuru Mkoani Tabora siku ya Ijumaa ( June 16) ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma.
Wadau kutoka Taasisi mbalimbali za Serikali, Mahakama, Polisi, Takukuru, Maliasili, Magereza, Halmashauri, Wakala wa Barabara,Mawakili wa Serikali na Wanasheria wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kwa kikao kazi cha majadiliano baina ya wadau hao na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambapo wameazimia kuzifanyia kazi changamoto mbalimbali zilizoibuliwa katika kikao hicho na kisha kupeana mrejesho.

Na Maura Mwingira, Tabora 

Katika kuadhimisha wiki ya Utumishi wa Umma, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali leo ( Juni 16) imekutana na wadau mbalimbali mkoani Tabora kwa madhumuni ya kujadiliana na kubadilishana mawazo yenye lengo la kuzitafutia ufumbuzi changamoto mbalimbali za kiutendaji.

Akitoa maelezo ya awali mbele ya wadau hao kutoka taasisi za serikali zinazofanya kazi kwa karibu na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Bw. Gerson Mdemu pamoja na mambo mengine amesisitiza haja na umuhimu kwa wadau hao pamoja na Ofisi yake kufanya kazi kwa ushirikiano wa karibu ili kuiwezesha serikali kutekeleza majukumu yake kwa ukamilifu.

“ Nyinyi ni wadau wetu muhimu sana sana, ni kwa sababu hiyo, katika wiki hii ya maadhimisho ya Utumishi wa Umma tukaamua kuja Mkoani Tabora ili tukutane nanyi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...