Mheshimiwa Freeman Mbowe(MB), Mwenyekiti wa Taifa, CHADEMA: 

NIMEPOKEA KWA MASIKITIKO NA HUZUNI KUBWA TAARIFA ZA KIFO CHA MZEE WETU MHESHIMIWA PHILEMON NDESAMBURO. NILIPATA BAHATI KUFANYA KAZI NA MZEE NDESAMBURO TUKIWA WABUNGE WA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA. 
BINAFSI NILIFAIDIKA SANA NA MAWAZO, HEKIMA, FIKRA, NA USHAURI WAKE KATIKA MASUALA MBALI MBALI YA KIBUNGE NA KITAIFA BILA KUJALI KWAMBA TULIKUWA VYAMA TOFAUTI.
PANDE ZOTE ZA BUNGE ZILIMTAMBUA NA KUMHESHIMU KWA UTULIVU WAKE NA HEKIMA KUBWA KATIKA KUWASILISHA HOJA ZAKE. 


KWA SABABU HIZO HAKIKA AMESAIDIA KATIKA KUJENGA NA KUIMARISHA DEMOKRASIA NCHINI. TAFADHALI TUFIKISHIE SALAAM ZANGU NA FAMILIA YANGU KWA FAMILIA YA MZEE NDESAMBURO NA WANA CHADEMA KWA KUMPOTEZA MUASISI NA MHIMILI WA CHAMA.
 KWA MWENYEZI MUNGU TULITOKA NA HAKIKA SOTE TUTARUDI KWAKE. MWENYEZI MUNGU AIREHEMU ROHO YA MAREHEMU NDESAMBURO. AMEEN.

Mark Mwandosya

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...