Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.
Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 21 Juni, 2017 amefuturisha wananchi wa mkoa
wa Pwani na kuwataka waumini wa dini ya Kiislam na madhehebu mengine kuendeleza
umoja na mshikano uliopo kwa muda mrefu kwa lengo la kudumisha amani nchini.
Mhe. Rais Magufuli amesema anaungana na waumini
wa dini ya Kiislamu nchini katika kumi la mwisho la Mwezi Mtukufu wa Ramadhani
kwa kuwaombea kumaliza kwa amani ibada ya Funga ya Ramadhani ikiwa ni
kutekeleza nguzo ya nne kati ya nguzo tano ya dini ya kiislam.
Amesema kwa mujibu wa dini ya Kiislamu ibada ya
Funga ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ni muhimu kwani ni njia sahihi ya
kujirekebisha kuachana na matendo maovu yanayoweza kusababisha kutenda dhambi.
‘’Ramadhani
ni ibada muhimu kwa Waislaam kwani ndio mwezi ambao huchoma dhambi zao na
kutenda matendo mema hivyo ni muhimu kwa ndugu Waislaam kuendeleza yote mema
ambayo wanafanya katika kipindi hiki cha mwezi wa Ramadhani ikiwa ni pamoja na
kuliombea Taifa.’’
Kwa upande wake Sheikh Mkuu wa Tanzania Mufti
Aboubakar Zubeir Ali ametaka wananchi wa Tanzania bila kujali itikadi za kidini
kuendelea kuliombea Taifa ili lizidi kuendelea kuwa na amani.
Nae Kaimu Sheikh wa mkoa wa Pwani Sheikh Hamisi
Mtupa amemshukuru Rais Magufuli kwa ukarimu wake wa kuwaaandalia futari
wananchi wa mkoa wa Pwani ikiwa ni pamoja na makundi maalum ya watoto yatima wa
kituo cha Bulome Foundation cha mjini Kibaha mkoani Pwani.
Jaffar Haniu
Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Kibaha, Pwani
Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiwa katika foleni ya kunawa na kisha kuchukua chakula leo Jumatano Juni 21, 2017 katika futari aliyowaandalia wananchi wa mkoa wa Pwani katika Ikulu ndogo ya Kibaha ambayo ilihudhuriwa pia na Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Aboubakar Zubeir Ali pamoja na viongozi wengine wa dini, serikali, vyama na watoto wanaolelewa kwenye vituo mbalimbali vya yatima mkoani humo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dkt John Pombe Magufuli (wa pili kulia) akichukua chakula leo Jumatano Juni 21, 2017 katika futali aliyowaandalia wananchi wa mkoa wa Pwani futari katika Ikulu ndogo ya Kibaha ambayo ilihudhuriwa pia na Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Aboubakar Zubeir Ali pamoja na viongozi wengine wa dini, serikali, vyama na watoto wanaolelewa kwenye vituo mbalimbali vya yatima mkoani humo.
Kina mama wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Kibaya Mhe. Asumpta Mshama wakichukua chakula wakati wa futari iliyoandaliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwa wananchi wa mkoa wa Pwani katika Ikulu ndogo ya Kibaha
Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akitoa neno la shukrani leo Jumatano Juni 21, 2017 wa waliohudhuria futari aliyowaandalia wananchi wa mkoa wa Pwani katika Ikulu ndogo ya Kibaha.
Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Aboubakar Zubeir Ali akizungumza machache na kuomba dua baada ya futari iliyoandaliwa na Rais Dkt John Pombe Magufuli kwa wananchi wa mkoa wa Pwani katika Ikulu ndogo ya Kibaha.
Sehemu ya waalikwa wakiitikia dua ikisomwa na Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Aboubakar Zubeir Ali baada ya futari iliyoandaliwa na Rais Dkt John Pombe Magufuli kwa wananchi wa mkoa wa Pwani katika Ikulu ndogo ya Kibaha.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...