Mkuu
wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Paul C. Makonda jana Alhamisi June 1, 2017
amemkabidhi Mwenge wa Uhuru Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist
Ndikilo katika dhifa ya Makabidhiano iliyofanyika katika Uwanja wa Ndege
wa Kimataifa wa Mwalimu J.K Nyerere Terminal 1 tayari kwa kuelekea
Mafia Mkoani Pwani.
Mwenge
wa Uhuru ni chombo kilichoasisiwa na baba wa Taifa Mwalimu Julius
Kambarage Nyerere mwaka 1961 ikiwa ni Tunu na ishara ya kuwepo kwa Taifa
huru la Tanganyika.
Akizungumza
wakati wa makabidhiano hayo Mhe Paul C. makonda amesema kuwa jumla ya
Miradi 40 imepitiwa na Mwenge wa Uhuru kwa Mwaka 2017 katika Mkoa wa
Dar es salaam yenye thamani ya Shilingi 244,392,530,334 huku akibainisha
kuwa Miradi 12 imezinduliwa, Miradi 15 imewekewa mawe ya Msingi, Miradi
miwili imefunguliwa na Miradi 11 imetembelewa.
Rc
Makonda alisema kuwa Mbio za Mwenge wa Uhuru tangu mwanzo zimekuwa
kichocheo kikubwa katika kuhamasisha Maendeleo , uzalendo, Umoja ,
Mshikamano na kudumisha Amani ndani na nje ya nchi.
Alisema
kuwa Mwenge wa Uhuru Mwaka 2017 wenye kauli mbiu isemayo Shiriki kukuza
uchumi wa viwanda kwa maendeleo ya nchi yetu pia umebeba jumbe
mbalimbali ikiwemo kupiga Vita Maambukizi mapya ya UKIMWI na Malaria
sambamba na kupiga Vita Matumizi ya Dawa za Kulevya.
Katika
mapambano dhidi ya Dawa za kulevya jitihada ya kudhibiti ni ajenda
muhimu kwa mustakabali wa maisha ya mtanzania kwa kuwa linagusa nguvu
kazi ya Taifa.
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo akizungumza mara baada ya kukabidhiwa Mwenge wa Uhuru na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Paul C. Makonda kwenye dhifa ya makabidhiano iliyofanyika katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu J.K Nyerere Terminal 1. jana Alhamisi June 1, 2017
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Paul C. Makonda akitoa taarifa ya Miradi iliyotembelewa na Mwenge wa Uhuru katika Mkoa wake mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo kwenye dhifa ya makabidhiano iliyofanyika katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu J.K Nyerere Terminal 1. jana Alhamisi June 1, 2017
Baadhi ya Wananchi waliozuru katika dhifa ya makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru iliyofanyika katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu J.K Nyerere Terminal 1. jana Alhamisi June 1, 2017
Viongozi mbalimbali wa serikali na wadau akiwemo Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo wakifatilia dhifa ya makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru iliyofanyika katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu J.K Nyerere Terminal 1. jana Alhamisi June 1, 2017.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...