Na Ripota wetu
Watalii wanaokuja Tanzania na kuelekea moja kwa moja kwenye hifadhi za taifa za Serengeti, Kilimanjaro au Ngorongoro inamaanisha nini? Ni kwamba wanakuwa wamekwishaambiwa kuwa ukifika Tanzania sehemu pekee za kutembelea ni hizo tu? Je tunawezaje kukabiliana na hali hii ambayo kwa namna moja ama nyingine inaweza kufifisha vivutio vilivyopo maeneo mengine nchini kutotembelewa?
Hakuna anayeweza kubisha kwamba sehemu ya Kaskazini mwa Tanzania imebarikiwa kwa kiasi kikubwa kuwa na vivutio visivyopatikana duniani kote. Vivutio kama hifadhi za kitaifa za Serengeti, bonge la Ngorongoro, Mlima Kilimanjaro na hivi karibuni mti mrefu zaidi barani Afrika uligunduliwa.

Tunapenda kukufahamisha kwamba tangu mwaka huu wa 2017 uanze nchi yetu imeshuhudia watu mbalimbali maarufu duniani wakifurika nyanda za Kaskazini wakiwemo Waziri Mkuu mstaafu wa Israel, Bw. Ehud Barak, muigizaji wa filamu kutokea Hollywood nchini Marekani, Will Smith na familia yake.

Kama hiyo haitoshi hazijapita hata wiki mbili tangu aliyekuwa nguli wa kusakata kabumbu nchini Uigereza, David Beckham ambaye aliwahi kuvichezea vilabu vya Manchester United, Real Madrid, LA Galaxy na PSG naye kutembelea hifadhi ya mbuga ya Serengeti akiwa na familia yake.

Huyo hakuwa mchezeji pekee kutokea bara la Ulaya kufanya hivyo kwani nyota anayechezea kwa mkopo katika klabu ya Crystal Palace inayoshiriki ligi kuu ya Uingereza akitokea Liverpool, Mamadou Sakho naye pamoja na mkewe na watoto wake wa kike wawili wameonekana wakifurahi mapumziko yao katika hifadhi ya mbuga ya wanyama ya Serengeti.

Jambo la msingi la kujiuliza hapa ni kwanini watu hao wote mashuhuri pindi tu watuapo uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwl. Nyerere hubadilisha ndege na kuelekea moja kwa moja uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro ambapo kutokea pale ni rahisi kwenda hifadhi za kitaifa za Serengeti, Ngorongoro na Mlima Kilimanjaro?

Tunafahamu kwamba suala la watalii kutembelea sehemu wanazozitaka wanapofika nchini Tanzania ni maamuzi yao na pia huchangiwa na sababu kadhaa kama vile vivutio miundombinu kama vile usafiri, hoteli zenye hadhi na kuvutia lakini pia na hali ya hewa kinaweza kuwa kigezo kingine.

Kwa kuzingatia sababu za miundombinu na huduma bora za malazi na zenye viwango vya kimataifa, hakuna ubishi kwamba nyanda za Kaskazini zimejitahidi kwa kiasi kikubwa kukidhi mahitaji ya watalii. Lakini linapokuja suala la vivutio vya kitalii na hali ya hewa bado Tanzania tumejaaliwa vivutio vya kila aina na hali ya hewa nzuri karibuni kila mikoa ya nchi hii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...