SERIKALI imesema kuwa
hakuna chombo chochote cha habari kitakachochukuliwa hatua kwa kuandika habari
zenye mrengo wa kukosa sera na utekelezaji wake kama ambavyo wadau wengi
wamekuwa wakiaminisha umma.
Kauli hiyo imetolewa
leo na Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo Dkt. Hassan Abbasi wakati
akizungumza katika Kipindi cha Habari Kuu kinachorushwa na Kituo cha Televisheni
cha Startv mjini Dodoma.
Dkt. Abbasi amesema
kuwa Sheria na 12 ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016 kifungu cha 51 kinatoa
ruhusa kwa chombo cha habari kukosoa kwa lengo la kuonyesha njia mbadala katika
kutatua changamoto zinazowakabili wananchi.
“Hakuna chombo cha
habari kitakachochukuliwa hatua kwa kukosoa, haki hiyo ipo kwa mujibu wa Sheria
ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016 kifungu cha 51, tutaendelea kuthamini na
kufanyia kazi ukosoaji huo,” alisema Dkt. Abbasi.Hata hivyo Dkt.
Abbasi amesisitiza kuwa Serikali haitasita kuchukua hatua kwa chombo
kitakachokiuka sheria na misingi ya maadili ya taaluma ya habari kwa lengo la
kulinda maslahi ya taifa.
Dkt. Amesisitiza kuwa
ni vyema wamiliki wa vyombo vya habari wakatumia uhuru huo wa kisheria kuchapisha
habari zenye nia njema kwa mustakabali wa maendeleo ya nchi badala ya kueneza
hofu miongoni ya mwa jamii.
Akijibu swali la
muongozaji wa Kipindi kuhusu kufungiwa kwa Gazeti la Mawio, Dkt. Abbasi amesema
kuwa Gazeti hilo halijafungiwa kutokana na kuandika habari ya kukosoa Serikali
isipokuwa limekiuka miiko ya taaluma kwa kuandika habari za kushushia heshima
na hadhi ya mtu katika jamii pamoja na kukiuka maagizo halali ya Serikali.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...