SERIKALI wilayani Korogwe Mkoani Tanga imepania kuhakikisha wanakomesha vitendo vya mimba za utotoni kwa kuwachukulia hatua kali watakaobinika kuhusika na matukio hayo ili kuweza kuondosha hali hiyo kwenye jamii.

Lakini pia imesema watakaohusika kuwa kichocheo cha ndoa hizo zifanyike wakiwemo wazazi kutoka pande zote mbili watafikishwa mahakamani ili sheria zichukue mkondo wake zaidi kwa lengo la kukomesha vitendo vya namna hiyo kwenye jamii.

Hayo yalibainishwa na Mkuu wa wilaya ya Korogwe ,Mhandisi,Robert Gabriel wakati makabidhiano ya vyumba vya madarasa vitano na vyoo ishirini na nne,mradi maji na uzio wa shule ya msingi jitengeni iliyopo Mji mdogo wa Mombo uliofanywa na taasisi isiyo ya kiserikali A better World ya Canada ikishirikiana na Vuga development Initiative
.
Alisema hatua hiyo ina lengo la kuhakikisha wanakomesha vitendo vinavyofanya na baadhi ya vijana vya kuwa sha wishi wananfunzi wa kike na kuwapatia ujauzito hivyo kupelekea wasichana hao kukatisha masomo yao.

Mkuu huyo wa wilaya alisema hivi sasa lazima wawe wakali na watu wanaocheza na maisha ya watoto ya wanafunzi ambao asilimia kubwa masomo yao yana haribiwa mara tu baada ya kushawishiwa na kupewa ujauzito.
MKUU wa wilaya ya Korogwe Mkoani Tanga,Mhandisi
Robert Gabriel akizungumza wakati makabidhiano ya vyumba vya madarasa vitano na vyoo ishirini na nne,mradi maji na uzio wa shule ya msingi jitengeni iliyopo Mji mdogo wa Mombo uliofanywa na taasisi isiyo ya kisherikali A better World ya Canada ikishirikiana na Vuga development Initiative kulia ni Founder wa A Better World Canada Eric Rajabu na Mkurugenzi wa Taasisi ya A Better Worild Canada
nchini Tanzania,Aizidi Kaoneka 
Founder wa A Better World Canada Eric Rajabu kushoto akizungumza katika halfa hiyo kulia ni Mkurugenzi wa Taasisi ya A Better Worild Canada nchini Tanzania,Aizidi Kaoneka 
Mkurugenzi wa Taasisi ya A Better Worild Canada nchini Tanzania,Aizidi Kaoneka akizungumza katika halfa hiyo 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...