Katika siku yake ya kwanza leo Jumamosi Tarehe 10 Juni 2017 Jijini Tanga, Sheikh Shariff Majini ametikisa jiji hilo kwa mkutano uliokusanya watu wengi katika ukumbi wa Community centre uliopo kitongojini Makorora.
Mkutano wa mwisho wa Sheikh Shariff utafanyika kesho Jumapili tarehe 11 Juni 2017 katika Ukumbi wa Xommunity Centre uliopo Makorora.
Mara baada ya kumalizika kwa mkutano huo Sheikh Shariff anataraji kurudi Dar es salaam tayari kwa kongamano la kina mama litakalofanyika ukumbi wa Star Light siku ya Jumamosi tarehe 24 Juni 2017.
Sheikh Shariff Majini akihutubia umati wa kinamama katika kongamano lake kwenye ukumbi wa Community centre uliopo kitongojini Makorora.
Sheikh Shariff Majini akiendelea na kongamano lake katika ukumbi wa Community centre uliopo kitongojini Makorora.
Sehemu ya umati wa kinamama katika kongamano la Sheikh Shariff Majani kwenye ukumbi wa Community centre uliopo kitongojini Makorora.
Sehemu ya umati wa kinamama katika kongamano la Sheikh Shariff Majani kwenye ukumbi wa Community centre uliopo kitongojini Makorora.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...