Meneja Miradi kutoka Social Action Trust Fund (SATF) Rogasian Massue akimkabidhi leo mfano wa hundi ya shilingi milioni 10 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi fedha ambazo zitatumika kwa ajili ya kulipia gharama za upasuaji wa moyo kwa watoto watano.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akimshukuru Meneja Miradi kutoka Social Action Trust Fund (SATF) Rogasian Massue mara baada ya kumkabidhi leo mfano wa hundi ya shilingi milioni 10 fedha ambazo zitatumika kwa ajili ya kulipia gharama za upasuaji wa moyo kwa watoto watano.
Meneja Miradi kutoka Social Action Trust Fund (SATF) Rogasian Massue akimsalimia mtoto Goodluck Msele ambaye amefanyiwa upasuaji wa moyo hivi karibuni katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na hali yake inaendelea vizuri. SATF imechangia shilingi milioni 10 fedha ambazo zitatumika kwa ajili ya kulipia gharama za upasuaji wa moyo kwa watoto watano.
Daktari Bingwa wa upasuaji wa Moyo kwa Watoto na Mkuu wa Idara ya Upasuaji wa Moyo kwa Watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Godwin Sharau (katikati) akimwelezea Meneja Miradi kutoka Social Action Trust Fund (SATF) Rogasian Massue (kushoto) kuhusu aina mbalimbali za magonjwa ya moyo yanayowasumbua watoto wanaotibiwa katika Taasisi hiyo. Kulia ni Msimamizi wa Wodi ya watoto Afisa Muuguzi Rogers Kibula.
Meneja Miradi kutoka Social Action Trust Fund (SATF) Rogasian Massue akimsikiliza Daktari Bingwa wa upasuaji wa Moyo kwa Watoto na Mkuu wa Idara ya Upasuaji wa Moyo kwa Watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Godwin Sharau wakati akimuelezea jinsi upasuaji wa moyo unavyofanyika katika Taasisi hiyo.Picha na JKCI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...