Na Humphrey Shao,Globu ya Jamii
Kampuni ya uuzaji wa vifaa vya Michezo ya ,Speshoz Tanzania imeingia mkataba wa kutoa vifaa vya Michezo  kwa timu ya Soka ya Lipuli ya Iringa ambayo imepanda kucheza ligi kuu ya Vodacom Tanzania.
Akizungumza wakati wa kusaini mkataba wa timu hiyo mkurugenzi wa Speshoz Tanzania,Jeffrey Jessey amesema mkataba huo ambao ni wa zaidi ya Milioni 30 utawawezesha kuuza jezi za Lipuli na kuwagawia vifaa vyote vya mazoezi.
“mkataba huu utaweza kuisadia timu hii kuwa na vifaa vya uhakika na vya kisasa ambavyo vitasaidia timu hiyo kuwa na morali na kuhimili ushindani na timu mkubwa” Amesema Jessey.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa timu ya Lipuli, Abu Changawa amesema kuwa mkataba huo ni moja ya vitu ambavyo vitasaidia timu hiyo kuwa na vifaa vya uhakika.
Amesema kuwa kampuni hiyo imewapa masharti kuwa timu hiyo ikifanikiwa kubaki sita bora basi wataongeza udhamini katika msimu ujao.
Changawa amesema  ni vyema makampuni mengine yakajitokeza kusaidia timu hiyo kwa upande wa udhamini hili iweze kufanya vizuri. 
 Mkurugenzi wa Kampuni ya Speshoz Tanzania Jeffrey Jessey akizungumza na Waandishi wa habari juu ya Mkataba wake na timu ya soka ya Lipuli ya Mkoani Iringa

 Mkurugenzi wa Kampuni ya Speshoz Tanzania ,Jeffrey Jessey  na  Mwenyekiti wa Lipuli Abu Changawa  wakisaini Mkataba wa Vifaa vya Michezo
Mkurugenzi wa Kampuni ya Speshoz Tanzania ,Jeffrey Jessey  na  Mwenyekiti wa Lipuli Abu Changawa  wakipeana mikono baada ya kusaini Mkataba wa Vifaa vya Michezo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...