Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai, pamoja na Mwenyekiti wa Mtandao wa Kuondoa Umasikini Ndg. Mungwe Athuman (kulia) wakimkabidhi  kitabu Kaimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Manghweta Ndg. Elinetha Kimaro (kushoto) wakati wakigawa vitabu Mbali mbali kwa Shule za Sekondari zilizopo Wilayani Kongwa Mkoani Dodoma. 
Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai (wa pili kulia) pamoja na Mwenyekiti wa Mtandao wa Kuondoa Umasikini Ndg. Mungwe Athumani (kulia) wakikabidhi vitabu kwa Mwl. Mkuu wa Shule ya sekondari Iduo Ndg. Cathbert Kalindo, Shule iliyopo Wilaya ni Kongwa Mkoani Dodoma.
 
 Spika wa Bunge Mhe Job  Ndugai (wa pili kushoto) akizungumza na Wazazi wa Wanafunzi wanaosoma katika Shule ya Sekondari Laikala iliyopo Wilayani Kongwa, Dodoma wakati wa zoezi la kugawa Vitabu shuleni hapo  vilivyotolewa na Mtandao Kuondoa Umasikini, kushoto ni Meneja wa Mtandao huo Ndg. Peter Yobwa.
   Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai (wa tatu kulia) akizungumza na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Ibwaga iliyopo Wilayani Kongwa, Dodoma baada ya kugawa vitabu shuleni hapo, vitabu hivyo  vimetolewa na Mtandao wa kuondoa Umasikini. Kulia kwa Spika ni Mweyekiti wa Mtandao huo Ndg. Mungwe Athuman  na kushoto kwake ni Meneja wa Mtandao huo Ndg. Peter Yobwa. Zoezi la ugwaji wa vitabu hivyo lilianza  toka wiki iliyopita ambapo takribani shule thelathini za Sekondari zilizopo Wilaya ya Kogwa, Dodoma zimenufaika na msaada huo. (Picha na Ofisi ya Bunge).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...