Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai akizungumza jambo kabla ya kuanza harambee kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Jumuiya ya kikristo Tanzania, tukio lililofanyika leo Mjini Dodoma. kushoto ni Waziri Mkuu Mstaafu, Mheshimiwa Mizengo Pinda na katikati ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya kikristo Tanzania, Askofu Dkt. Alex Malasusa
Waziri Mkuu Mstaafu, Mheshimiwa Mizengo Pinda (wa pili kushoto) akizungumza jambo baada ya kumalizika kwa harambee kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Jumuiya ya kikristo Tanzania, kulia ni Katibu wa Bunge, Dkt. Thomas Kashililah, kushoto ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya kikristo Tanzania, Askofu Dkt. Alex Malasusa na wa pili kulia ni Ndg. Elton Mapesa Mwakilishi wa Harambee kutoka External Ubungo Jijini Dar es Salaam.
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kulia) akisalimiana na Mwenyekiti wa Jumuiya ya kikristo Tanzania, Askofu Dkt. Alex Malasusa kabla ya kuanza harambee kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Jumuiya ya kikristo Tanzania, katika tukio lililofanyika leo Mjini Dodoma, Spika Ndugai pia ni Mgeni rasmi na aliongoza Wabunge katika harambee hiyo.
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (wa pili kulia)akiongoza Wabunge Mbali mbali kucheza nyimbo ya injili kama njia moja wapo ya kuhamasisha uchangiaji kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Jumuiya ya kikristo Tanzania, tukio lililofanyika leo Mjini Dodoma
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...