Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

MASHINDANO ya Sprite Bball Kings 2017 yanaendelea tena wikiendi hii kwa michezo mitano kupigwa katika

Viwanja vya Bandari, Mivinjeni huku washindi wa jumla wa mechi hizo wataungana na wa wiki iliyopita.

Hii ni wiki ya tatu toka kuanza kwa mashindano hayo ikizikutanisha timu 52 kutoka sehemu mbaalimbali za Mkoa wa Dar es Salaam.Katika michezo ya wiki hii.

Katika wiki hii, kutakuwa na michezo mitano itakayowakutanisha Ukonga Warrior dhidi ya Mchenga Team, Heroes B dhidi ya Ardhi University na mechi ya tatu ni kati ya Flying Dribblers na UDSM.
Mechi ya nne ni kati ya Kigamboni Heroes na St Lous Montfort huku DMI wakivaana na nOsterbay michezo itakayoanza mida ya saa 2 asubuhi mpaka sa 12 jioni.


Mratibu wa mashindano hayo ya Sprite Bball Kings 2017 Basilisa Basike amesema hii ni muendelezo wa hatua ya pili baada ya wiki iliyopita kuchezwa kwa mechi nne na zingine tano zinamalizika wikiendi hii.


"Baada ya michezo hiyo, washindi wa jumla wataungana na wale wa wiki iliyopita na tutachezesha droo ya timu zitakazokutana ili kuingia hatua ya tatu ya Sprite Bball Kings 2017," amesema Basilisa.

Michuano hiyo inayodhaminiwa na Sprite kwa kushirikiana na East Africa Tv na Redio inaendelea tena wikiendi hii katika viwanja vya Bandari, Mivinjeni  na mshindi kamili ataondoka na kitita cha shiling milion 15.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...