Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Alhad Mussa Salum amewatangazia waumini wa dini ya kiislam kuwa Swala ya eid El fitri itaswaliwa mnamo siku ya jumatatu Juni 26, 2017 katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es salaam, ikiwa ni baada ya kukamilika mfungo mtukufu wa mwezi wa Ramadhani.

Sheikh Salum aliyazungumza hayo jana wakati wa mkutano wake na waandishi wa habari, na amewataka na kuwaasa waumini wa kiislam kuhakikisha wanatekeleza mema yote kama waliyokuwa wakiyafanya katika mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Akizungumzia siku ya ibada hiyo muhimu kwa waislam wote ulimwenguni, Sheikh Salum alimesema katika viwanja vya mnazi wageni mbali mbali wanatarajiwa kuwepo, lakini pia mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais Mstaafu wa awamu ya pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Alhaj Ali Hassan Mwinyi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Ana uhakika gani kama mwezi hautoandama mwezi 29??

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...