Familia ya Bw.  Byabato wa Kinondoni, Morroco Dar es salaam inasikitika kutangaza kifo cha baba yao mpendwa Bw. Francis Byabato kilichotokea tar 12 June katika hospitali ya Muhimbili Dar es salaam. Miaka ya Awali,  Marehemu alifanya kazi na kampuni ya East African Community Nairobi na Arusha,  na katika ofisi ya Hazina ( Treasury) Dar es salaam. Baada ya kustaafu alianzisha biashara  kampuni ya Bureau de Change jijini Dar es salam.

Marehemu ameacha Mke wake Mpendwa. Demetria Byabato wa Kinondoni, Dar es salaam, pamoja na wanae --Digna Byabato- Makobore (Daudi) wa Mikocheni, Dar es salaam, Alvera Byabato- Ijumba (Edmund) wa Memphis, Tennessee, Hilda Byabato Curry (Reginald) wa Frisco, Texas, William Byabato wa Mikocheni Dar es salaam na Robert Byabato (Delilah) wa Frisco, Texas: Pamoja na Wajukuu Dorothy, Daniel, Kendra, Ingrid, Ethan, Adoree, Jayden, Robert Jr., Isabella na Braxton.
Dada zake Tereza, Leonida  na Maria.

Mazishi yatafanyika Bwanjai, Bukoba, ijumaa, June 16. Kutakuwa na misa ya kumuaga marehemu jumatano tarehe 14, saa sita mchana katika kanisa la St Peters, Oysterbay, Dar es salaam.

Bwana ametoa, Bwana ametwaa. Jina la bwana libarikiwe.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...