ESTER NAPENDA MFINANGA
(1952 – 2017)
Kwa niaba ya wanandugu wote Ndugu Boniface
A. Mfinanga wa Chanjale, Kisangara Mwanga Kilimanjaro anayo heshima kubwa kutoa
shukrani za dhati kabisa kwa ndugu, jamaa na marafiki ambao walishiriki kwa
namna moja au nyingine katika kufanikisha mazishi ya mama yao mpendwa, ESTER
NAPENDA MFINANGA aliyefariki dunia siku ya tarehe 13/4/2017 Neema Roman
Catholic Health Centre Mwanga na kuzikwa kijijini kwao Chanjale, Kisangara, Mwanga,
Kilimanjaro tarehe 17/4/2017
Kwa vile mlioungana nasi kwa kutufariji wakati wa kipindi chote cha msiba huu
mkubwa ni wengi na ni vigumu kuwataja wote kwa majina, kama familia tunapenda
kwa heshima kubwa kutoa shukrani za jumla tukiwaomba wote mkubali kuzipokea kwa
moyo ule ule kama mlivyotuunga mkono. Mmetufariji sana, mmekesha nasi,
mmeshinda nasi, nyote mmekuwa kimbilio salama kwetu wakati wa kipindi hiki
kigumu. Mlionyesha upendo wa kweli kwetu kama familia na kwa mama yetu
mpendwa.
Tunapenda kutoa shukurani za kipekee kwa marafiki na wanandugu ambao michango yao itabakia
kwa familia na nyoyo za watoto wa marehemu tukianza na Ndugu wote, majirani na
marafiki wa karibu kutoka Mwanga,
Kisangara, Lembeni, Kifaru, Kiruru, Kilomeni, Soffe, Kisangara juu, Same, Pongwe
Tanga, Bukoba, Moshi, Arusha, Mwanza na Dar es Salaam, kweli michango yenu
kamwe haitasahaulika.
Familia pia inapenda kuwashukuru Baba
askofu mstahafu Jacob Koda, Baba Paroko wa Parokia ya Chanjale Samwel Lawena,
Padre Peter Mvungi, Padre Valence Sewangi, na Padre Anthony Mmari kwa
kutuongozea misa takatifu ya kumpumzisha mama yetu mpendwa katika nyumba yake
ya milele.
Familia vile vile inapenda kutoa shukrani za dhati kabisa kwa Dr Avelin Kimario
na Dr Swai pamoja na manesi Prisca Silayo, Prediganda
Kimario, Lightness Mduma, Donatila Msuya na Vaileth Mdee wa NEEMA ROMAN CATHOLIC HEALTH CENTRE Mwanga,
Kilimanjaro kwa juhudi zao za dhati kabisa
za kutaka kuokoa maisha ya mama yetu mpendwa.
Aidha, tunatoa shukrani kwa wafanyakazi na uongozi wa TANAPA Arusha, MSD Tanga
na Bukoba, South African High Commission Dar es Salaam Mission, Murhandzwa Ltd,
Tanganyika Arms Ltd, Ndugu Marwa Issa wa Kiliflora Ltd, Ndugu Gabin Msuya na
wafanyakazi wote wa MSUYA AUTO GARAGE Mwanga, Wanajumuiya wa Mashahidi wa
Uganda kanisa la Kristo Mfalme Moshi, Wanajumuiya ya Mt. Petro parokia ya
Mwanga, Magrooup yote ya WhatsApp ya wanandugu na marafiki kwa michango yenu iliyotufariji, tutaendelea kukumbuka ukarimu
wenu daima.
Vile vile familia inawashukuru sana majirani wa Mwanga, Chanjale, Kisangara kwa
kushiriki na kushughulika kwa heshima zote katika msiba wa Mama yetu mpendwa.
Mwisho Tunawashukuru wote mlioweza kufika nyumbani Chanjale, Kisangara Mwanga na
kumhifadhi Mama yetu mpendwa ESTER NAPENDA MFINANGA katika nyumba
yake ya milele. Hatuna cha kuwalipa, Mungu atawalipa zaidi na zaidi.
Mama utakumbukwa daima na wanafamilia
wote, Kaka na dada zako, shangazi, na wanao woote hususani Boniface, Bona, Yukunda, Bruno, Dorice, Luciana, Anastazia (Team Napenda)
na wajukuu wako woote hususani Nice,
Ester, Anatoly, Primi, Laris na Emmilyne
Quotes from Mom
1. “MUWASAMEHE MADHAMBI YAO NA MUWAPENDE”
2. “MGURANE”
BWANA ALITOA BWANA AMETWAA, JINA LA BWANA LIHIMIDIWE
AMEN
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...