Kaimu Hakimu Mkazi-Mfawidhi, Mahakama ya Hakimu Mkazi-Njombe, Mhe. Paul Kapokolo akiwa ofisini kwake mkoani Njombe, Mhe. Kapokolo ambaye pia ni Hakimu Mkazi Mfawidhi, Mahakama ya Wilaya Njombe amesema Mahakama mkoani Njombe imejiwekea mikakati ya kushughulikia mashauri kwa wakati ikiwa ni pamoja na kufanya vikao vya kusukuma mashauri (case flow management) ili kupata ufumbuzi kwa mashauri yanayoonekana kukwama, kuhimiza Waendesha Mashitaka/Polisi kuleta mashahidi kwa kila tarehe wanayopangiwa kusikiliza mashauri n.k
 Mtendaji, Mahakama ya Hakimu Mkazi-Njombe, Bi. Maria Francis Itala, Bi. Itala alisema kuwa Mahakama mkoani Njombe wanakabiliwa na tatizo kubwa la upungufu wa Watumishi wa Kada mbalimbali, alisema kwa sasa Mkoa huo una jumla ya Watumishi 78 na uhitaji wa Watumishi ili kutekeleza Majukumu tofauti tofauti ni 359, na hivyo kufanya kuwa na upungufu wa Watumishi 28.
 Mhe. Isaya, wa kwanza kulia akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Watumishi wa Mahakama ya Mwanzo-Kalenga, wa kwanza kushoto ni Hakimu Mkazi Mfawidhi-Mahakama ya Mwanzo-Kalenga, Mhe. Magdalena Malaba.
Hakimu Mkazi Mfawidhi, Mahakama ya Wilaya-Iringa, Mhe. Isaya Godfrey akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Mahakama ya Mwanzo Kalenga mara baada ya kukamilisha shughuli ya ukaguzi iliyompeleka katika Mahakama hiyo. (Picha na Mary Gwera, Mahakama)



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...