Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.

Tatizo la ugonjwa   wa macho katika nchi ni kubwa ambalo linachangiwa kwa kukosa rasilimali watu pamoja na vifaa vya kisasa katika kutatua changamoto hiyo.

Akizungumza katika kikao cha wadau wanaoshughulika na masuala ya macho kilichoandaliwa na Sightsavers , Kaimu Meneja wa Mpango wa Taifa wa Huduma za Macho wa Wizara ya Afya , Maendeleo ya Jamii , Jinsia , Wazee na Watoto, Dk. Bernadetha Shilio amesema tatizo la macho ni dogo katika nchi lakini kutokana na kukosa kwa rasilimali watu pamoja na vifaa vya kufanyia oparesheni linafanya tatizo kuwa kubwa.

Amesema kutokana na tatizo la ugonjwa wa macho kuwa kubwa wameandaa mikakati ya kutatua,ikiwemo kuongeza rasilimali watu pamoja na vitendea kazi kwa ajili ya kufanyia operesheni.

Dkt.Bernadetha amesema kuwa kuna ushirikiano na mashirika mbalimbali katika yanayosaidia kutoa huduma ya ugonjwa wa macho katika sehemu mbalimbali nchini.Mkurugenzi Mkazi wa Sightsavers, Gosbart Katuzi amesema kuwa tatizo la ugonjwa wa macho unatokana na kitoto cha jicho na kufanya wengine kupofoka.

Amesema kuwa katika mradi mwaka 2009 walipeleka vifaa katika mkoa morogoro ambapo katika kliniki hiyo zaidi watu 12000 walibainika kuwa na ugonjwa wa macho.Katuzi amesema kuwa kwa sasa ya watu milioni moja wana matatizo ya macho hali hiyo jitihada zinatakiwa kufanyika katika kuifikia idadi hiyo ambayo itakuwa ikiongezeka kwa kila mwaka.

Mkurugenzi wa Help Age International, Smart Daniel amesema ugonjwa wa macho umekuwa ukiwakumba wazee ambapo hushindwa kufanya kazi zao kutokana na ugonjwa wa macho.

Amesema kuwa kuna jitihada ambazo zimekuwa zikifanyika katika  kuwafikia wenye ugonjwa macho na watu wengine kwa kufanyiwa oparesheni.
Kaimu Meneja wa Mapngo wa Taifa wa Huduma za Macho wa Wizara ya Afya , Maendeleo ya Jamii , Jinsia , Wazee na Watoto, Dk. Bernadetha Shilio akizungumza katika kikao juu wadau wanashughulika na ugonjwa wa macho leo jijini Dar es Salaam.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Sightsavers, Caroline Harper akizungumza juu ya taasisi hiyo ilivyoweza kusaidia maeneo mbalimbali nchini kwa watu wenye ugonjwa macho leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Help Age International, Smart Daniel akizungumza katika mkutano wa wadau wanaoshughulika na ugonjwa macho juu ya wazee walivyokuwa wahanga wa ugonjwa huo leo jijini Dar es Salaam.
Afisa Mahusiano na Masoko wa Standard Chartered ,Juanita Mramba akizungumza juu ya utoaji wa msaada wa benki hiyo kwa watu wenye ugonjwa wa macho leo jijini Dar es Salaam
Wadau wa wanaoshulika na ugonjwa wa macho wakiwa katika picha pamoja leo jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...