Frank Mvungi-Maelezo 

Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) imezindua mkataba wa huduma kwa wateja ikiwa ni nyenzo mojawapo inayowezesha kutolewa kwa huduma bora katika kiwango cha kimataifa na kutekelezwa kwa vitendo juhudi za Serikali katika kuwahudumia wananchi kwa weledi na uwajibikaji.

Kauli hiyo imetolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Tiba Dkt. Doroth Gwajima wakati akizindua mkataba wa huduma kwa wateja wa Mamlaka hiyo leo Jijini Dar es Salaam kwa niaba ya Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu.

Akizungumza kuhusu mkataba huo Dkt. Gwajima amesema kuwa ni jambo la faraja kuona kwamba uzinduzi wa mkataba huu unafanyika katika kipindi cha maadhimisho ya wiki ya utumishi wa umma mwaka 2017 ambayo msingi wake ni kutoa huduma bora zinazoridhisha wateja kwa kuzingatia mkataba shirikishi wa huduma kwa wateja.

“Nawapongeza TFDA kwani kwa kutekeleza mkataba huu,watumishi wataweza kuepuka uzembe,upendeleo, na rushwa mambo ambayo husababisha malalamiko kwa wananchi dhidi ya watumishi na Serikali yao” Alisisitiza Gwajima.

Akifafanua amesema mkataba huo utawezesha wateja kutambua haki zao, wajibu wao hali itakayosaidia TFDA kuweka mfumo dhabiti wa upimaji wa viwango vya huduma (service standards) kwa mujibu wa mkataba ili kubaini ufanisi wa mkataba huu na kuchukua hatua stahiki za uboreshaji wa huduma pale inapobidi.

Aidha, alipongeza TFDA kwa kuweka namba ya simu ambayo mteja anapiga bure wakati wa kazi, kuhusiana na huduma zinazotolewa na TFDA ambayo ni 0800110084 na kuitumia inavyostaili. 
 Kaimu Mkurugenzi wa Tiba toka Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na watoto Dkt. Doroth Gwajima (katikati) akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi mkataba wa huduma kwa wateja wa Mamlaka hiyo leo Jijini  Dar es Salaam  kwa niaba ya Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu.
 Kaimu Mkurugenzi wa Tiba toka Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na watoto Dkt. Doroth Gwajima (katikati) akionesha mkataba wa huduma kwa wateja wa TFDA mara baada ya kuuzindua leo Jijini Dar es Salaam.kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA ) Bw. Hiiti Sillo na kushoto Mkurugenzi wa Idara ya Uchambuzi na Usahuri wa kazi toka Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora Bw. Mick Kiliba. 
 . Kaimu Mkurugenzi wa Tiba toka Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na watoto Dkt. Doroth Gwajima akikata utepe kuzindua namba maalum itakayotumiwa na wananchi kuwasilina na Mamlaka hiyo ikiwa ni sehemu ya uzinduzi wa mkataba wa huduma kwa wateja.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...