Kamishina wa Bima, Dr.Baghayo Saqware akizungumza na wadau mbalimbali wa masuala ya bima mkoa wa Mbeya katika uzinduzi wa mfumo mpya wa kielectroniki kuhakiki uhalali wa Stika za Bima.

Uzinduzi wa kukaguwa na kuhakiki stika za bima uliofanyika katika ukumbi mdogo wa mkapa jijini mbeya kwa lengo la kupeleka elimu zaidi mtaani kwa watumiaji wa vyombo vya moto ikiwemo magari, pikipiki, bajaji na kadhalika, juu ya kujikinga na majanga mbalimbali ya tokanayo na ajari za barabarani pamoja na wezi, na mahalamia wa wa bima feki.

Bima hii yenyekulenga kuepusha ajari mbalimbali za barabarani kutoka katika kampuni ya bima ya (TIRA) “Tanzania Insurance Regulatory Authority” pia  imetoa huduma hii ya kwa mfumo wa kisasa wa kuhakiki bima kupitia simu ya mkononi kwa kushirikiana na kampuni mbili za mtandao wa simu, Tigo na Vodacom Tanzania kwa njia ya ujumbe mfupi wa maandishi (SMS) na Kwa Intanenti.
Waweza kuhakiki bima yako kwa kupitia mitandao ya simu (TIGO na VODACOM) kwa kwenda kwenye uwanja wa ujumbe mfupi wa simu ya mkononi  kwa kuandika neno STIKA acha nafasi kisha Andika Namba ya Stika i.e STIKA 8091390, kisha itume kwenda nambari 15200 ambapo utatozwa shilingi Mia Moja (100) Tu.
Kupitia Intanenti waweza kwenda kwenye Tovuti ya TIRA MIS https://mis.tira.go.tz, Kisha bofya Hakiki Stika za Bima/Validate Motor Insurance Sticker, kisha ingiza namba ya stika na bofya Hakiki/Validate.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya, Dhahiri Kidavashari nae akichangia machache katika uzinduzi huo wa  mfumo mpya wa kielectroniki kuhakiki uhalali wa Stika za Bima.
Zoezi la uhakiki likiendelea kuanzia hii leo barabarani hivyo wamiliki wote wa vyombo vya usafiri kuimizwa kuhakiki Stika za Bima kwenye vyombo vyao.
Moja kati ya wadau wa Bima akifuatilia kwa makini semina ya Kamishna wa Bima Tanzania katika ukumbi wa mkapa Jijini Mbeya leo. 
PICHA ZOTE NA MR.PENGO MBEYA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...