NA HAJI NASSOR, PEMBA

TUME ya kurekebisha sheria Zanzibar, imeanza zoezi la kuwasilisha miswada mitatu ya sheria ikiwemo ya uharibifu wa mazao, kwa wadau mbali mbali kisiwani Pemba, baada ya kukusanya maoni ya marekebisho ya sheria hizo, miezi iliopita.

Awali tume hiyo chini ya Mwenyekiti Jaji Mshibe Ali Bakari na Katibu wake Asma Jidawi, walipita kwa wadau mbali mbali wakiwemo masheha, wanasheria, wakulima na wananchi wengine kukusanya maoni, ili kuzifanyia marekebisho sheria hizo kongwe.

Akiwasilisha mswada ya sheria ya Uharibifu wa mazao, mwanasheria kutoka Tume hiyo Tajo Ameri alisema, kwa sasa baada ya maoni ya wananchi, sheria inayokuja inatmbua uharibifu wa mazao mbali mbali, badala ya ile ya zamani kuwa na mazao aina mbili pekee.

Alisema, jengine ambalo limo kwenye mswada huo ni kuingizwa kwa mazao hata yanayotoka nje ya Zanzibar, ambapo mawali sheria hiyo ya uharibifu wa mazao, ilitambua yale yanayozaliwa nchini pekee.

“Tulipita Unguja na Pemba kwa wadau mbali mbali, ili kukusanya maoni juu ya sheria ya uharibifu wa mazao, na sasa tunayarejesha tena kwenu ili kuona kama mliotueleza ndio”,alifafanua.

Kwa upande wake, mwanasheria wa Tume hiyo Miwta Khamis Haji, alisema, suala la usajili wa nyaraka limekuwa ni jambo la lazima kwa mali, kama vile mashamba na nyumba, ili kuondoa udanganyifu unaoweza kujitokeza.

Mapema Katibu wa Tume hiyo ya Kurekebisha Sheria Zanzibar, Asma Jidawi, alisema miongoni mwa kazi kubwa ya tume hiyo, ni kuzifanyia marekebisho sheria au vifungu ambavyo vinaonekana kupitwa na wakati.

Hata hivyo aliwataka wananchi na wadau wengine, kuendelea kutoa maeoni yao kwa sheria mbali mbali, ambazo tume hiyo huzifanyia marekebisho.

Baadhi ya masheha waliohudhuria mkutano huo, walisema elimu ya usajili wa mali, nyaraka na ardhi inahitajika ili wananchi wapate elimu ya kutekeleza sheria.

Shehe wa shehia ya Mgelema Omar Idd Zaina, alisema bado migogoro ya ardhi hujitokeza kwa baadhi ya wamiliki kutokana na kukosa uwelewa juu ya umuhimu wa kusajili ardhi zao.

Nae Sheha wa shehia ya Uweleni Abdalla Omar Mjawiri, aliipongeza Tume hiyo, kutokana na kuwarejeshea maoni yao walioyakusanya wakati zikifanyia marekebisho sheria za uharibifu wa mazao, usajili wa nyaraka na sheria ya endelevu ya ardhi.

Tayari Tume ya Kurekebisha sheria Zanzibar imeshazifanyia marekebisho sheria 17 ikiwemo sheria ya ushahidi, sheria ya wanyama, vileo na sheria ya usafirishaji baharini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...