Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

KOCHA msaidizi wa timu ya Mtibwa Zuberi Katwila amesema kuwa kwa sasa anasubiri maamuzi ya Mwenyekiti wa klabu hiyo baada ya kumkabidhi ripoti ya mwaka mzima ya kikosi hicho.

Akizugumza na Mtandao huu, Katwila amesema kuwa ameshakabidhi ripoti kwa Uongozi wa klabu hiyo  na wanatarajiwa kuanza maezoezi Julai mosi mwaka huu kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya wa 2017/18.

Katwila amesema, hawezi kuweka wazi ni wachezaji gani watakaoachwa ila ripoti nzima imeweka wazi wachezaji wanaohitajika kuachwa na sababu zao kwani kila mmoja amewekewa muda aliocheza na alicheza katika kiwango cha juu au chini.

"kila mchezaji ameainishwa katika ripoti katika vipengele tofauti kama aliweza kucheza kwa muda gani na kwa kiwango gani, mbali na hilo wapo ambao wameshindwa kuonyesha kiwango kikubwa na pia nao nimewaandikia sababu za kuachwa,"alisema Katwila.

Amesema, ukiachilia hilo pia katika ripoti yake ameweka wazi wachezaji anaowahitaji ila cha zaidi anasubiri majibu ya uongozi kuhusiana na wachezaji hao na iwapo watashindikana kupatikana hatua ya itakayofuata ni kuita wachezaji katika kufanya majaribio katika timu yao.

Katwila amesema mpaka sasa hawajajua ni wapi wataweka kambi hiyo ya maandalizi ya ligi hadi pale watakapopata maelekezo kutoka kwa Uongozi kama watakaa Manungu au nje ya mkoa wa Morogoro.


Kikosi cha Mtibwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...