NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR.

UMOJA wa Wanawake wa Chama cha Mapinduzi  Tanzania (UWT)  umewataka wanawake kuchangamkia fursa za Uongozi wa ngazi mbali mbali  kupitia uchaguzi unaondelea hivi sasa ndani ya Chama na jumuiya zake.

Wito huo umetolewa Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja huo Zanzibar  Bi.Tunu Juma Kondo    katika mwendelezo wa ziara ya  UWT  ya kuzungumza na Viongozi wapya wa ngazi za matawi wa umoja huo uko Jimbo la Kijini  Wilaya ya Kaskazini "A"  kichama Unguja.

Awambia  Akina Mama hao kuwa Uchaguzi  wa ngazi mbali mbali unaoendelea  katika taasisi hiyo ndio fursa moja wapo ya wanawake  kupata nafasi za uongozi ili waweze kufikia malengo ya kupata uwakilishi wa viongozi wenye idadi sawa na wanaume ndani ya Chama hicho.

Alifafanua kuwa wanawake wanatakiwa kuondokana na dhana ya kuendelea  kuongozwa kwa kila nafasi za uongozi ndani ya CCM bali wanatakiwa kujiongeza kwa kuwania wenyewe uongozi ndani ya chama hicho ili kuleta maendeleo endelevu ndani ya chama na jumuiya zake.

Pia alisisitiza viongozi hao kuwa pamoja na majukumu ya kiuongozi waliyonayo ni lazima wawahamasishe  kwa wingi wanawake  kuwania nafasi za uongozi ili kupata viongozi makini na wenye  uwezo  wa kwenda na kasi  za kiutendaji za chama hicho.

"Wanawake wenzangu tutumieni fursa ya Uchaguzi wa Chama kuwania nafasi mbali mbali za uongozi , tusisubiri nafasi za uteuzi  bali tusimame wenyewe  kupambana kwa kuhakikisha nasi tunakuwa na nyadhifa za uongozi kama walivyo wanaume kwani tunaweza wenyewe bila ya kuwezeshwa’’,. Alisema Bi.Tunu.
 Kaimu  Naibu  Mkuu wa UWT Zanzibar, Bi. Tunu Juma Kondo akizungumza na viongozi wa Matawi ya Jimbo Kijini Wilaya ya Kaskazini “A” kichama Unguja.
  Katibu Msaidizi wa  Idara ya  Organazesheni  UWT Zanzibar, Bi. Mgeni  Ottow akitoa nasaha kwa viongozi wa Matawi ya Jimbo Kijini Wilaya ya Kaskazini “A” kichama Unguja.
Baadhi ya viongozi wa UWT  wa Matawi jimbo la kijini Wilaya ya Kaskazini “A”  kichama Unguja wakisikiliza kwa makini nasaha zinazotolewa na viongozi wa UWT Zanzibar  uko Tawi la CCM Muange.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...