Na. Frank Mvungi - Maelezo
Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) imeandaa mkakati wa
kuwasaidia wajasiriamali nchini kukabiriana na changamoto
zinazokwamisha maendeleo yao ili waweze kuchangia juhudi za Serikali
katika kujenga uchumi wa viwanda.
Mkurugenzi wa TFDA, Bw. Hiiti Sillo ameeleza hivi karibuni kuwa miongoni
mwa mikakati hiyo ni pamoja na kutoa mafunzo ya ujasiliamali kwa
kushirikiana na taasisi zingine ambazo kwa njia moja au nyingine zinagusa
shughuli za wajasiliamali nchini.
Alizitaja taasisi hizo kuwa ni Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Shirika la
Maendeleo ya Viwanda Vidogo (SIDO) na Mamlaka ya Maendeleo ya
Biashara Tanzania (Tantrade) na GS1, ambazo kwa pamoja zitakuwa
zikitoa mafunzo ya namna ya kuboresha bidhaa za wajasiriamali ili
ziendande na mahitaji ya soko la ndani na nje ya nchi.
“Changamoto zinazowakabili wajasiriamali ni mtambuka na zinahitaji
mikakati ya pamoja ya sekta na wadau katika kukabiliana nazo”.
Alisisitiza Sillo wakati wa kikao cha pamoja na taasisi hizo.
Ametaja mkakati mwingine ni kuundwa kwa Kamati ya wataalam nane
ambayo itaratibu namna ya kutekeleza mikakati ya kuondoa changamoto
zinazowakabili wajasiriamali kote nchini. Kamati hiyo itajumuisha
wajumbe wawili kutoka kila taasisi.
Pia Bw. Sillo amezishauri TanTrade na SIDO kufuatilia katika halmashauri
zote nchini upatikanaji wa maeneo ya uzalishaji yatakayotumiwa na
wajasiriamali hao ili kutekeleza dhana ya ujenzi wa uchumi wa viwanda
kwa vitendo.
Kwa upande wa bidhaa hatarishi (high risk food products), Mkurugenzi wa
TFDA amesisiza bidhaa hizo zisizalishwe bila kuwa na vibali kutoka TFDA
ili kulinda afya ya mlaji na mamlaka hiyo kufanya marejeo ya kanuni ya
ada na tozo ni mkakati wa kuweka unafuu kwa wajasiriamali.
Kuanzia mwaka 2013/14 hadi 2016/17, TFDA imetoa mafunzo kwa
wajasiliamali katika mikoa 16 ambayo ni Dar es Slaam, Pwani, Mwanza,
Arusha, Mbeya, Dodoma na Rukwa.
Mikoa mingine ni Manyara, Lindi, Mtwara, Tanga, Singida, Iringa, Kigoma,
Kilimanjaro na Morogoro.
Aidha jumla ya wajasiriamali 1,287 wameisha pewa mafunzo mapaka
kufikia mwezi June, 2017 ambapo kwa sasa mafunzo hayo yatafanyika
kwa kushirikisha taasisi zote zenye jukumu la kuwahudumia wajasiriamali
hapa nchini.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) bw. Hiiti Sillo
akizungumza wakati wa Kikao cha pamoja kati kati ya Shirika la Viwango Tanzania
(TBS),SIDO,TANTRADE kilichofanyika hivi karibuni kikilenga kuweka mikakati ya
pamoja itakayosaidia kutatua changamoto zinazowakabili wajasiriamali hapa
nchini.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) bw. Hiiti Sillo
wakwanza kutoka kushoto akiwa katika picha ya pamoja na Muwakilishi wa
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) Mhandisi Agnes Kiwelu
(katikati) na Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa SIDO Prof. Sylvester Mpanduji na
mwisho kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TANTRADE Bw. Edwin Rutagarika.
(Picha na TFDA).
Mnawasaidia kina nani watu wakija ofisini kwenu hakuna ushirikiano mnawapa zaidi ya kuwafanya waone biashara ya food processing ni ngumu,nyie mlitakiwa muwe na link na watu walosomea food processing ili mtu anapotaka kufungua kiwanda hao watu wanapatikana kwenu,tatizo tukija kuchukua fomu zenu watu wa food processing tukawatafute sisi tunawatoa wapi
ReplyDelete