Na Dotto Mwaibale
WAKINA Baba nchini wametakiwa kutoa elimu ya afya ya uzazi kwa watoto wao badala ya kuwaachia kazi hiyo ifanywe na wakina mama pekee.
Mwito huo umetolewa na Selemani Bishagazi wakati akichangia mada katika kongamano la siku moja lililohusu elimu ya afya ya uzazi kwa watoto hasa wa kike lililoandaliwa na TGNP Mtandao jijini Dar es Salaam jana.
"Suala la utoaji wa elimu ya afya ya uzazi kwa watoto wetu hasa wa kike ni letu sote kati ya baba na mama kwani baba ndie chanzo kikubwa cha mapato katika familia" alisema Bishagazi.
Bishagazi alisema suala la kutoa fedha za kunulia pedi wakati mtoto wa kike anapokuwa kwenye hedhi si la mama bali hata baba anawajibu wa kutoa fedha hizo na akaomba dhana hiyo potofu kuwa mama ndiye anawajibika katika suala hilo iachwe.
Ofisa Programu wa TGNP Mtandao, Anna Sangai (kushoto), akitoa mada katika kongamano la siku moja lililohusu elimu ya afya ya uzazi lililofanyika Makao Makuu ya TGNP Mabibo Dar es Salaam jana. Kongamano hilo liliandaliwa na TGNP.
Mwanafunzi Leila Kisinga kutoka Sekondari ya Mabibo akitoa mada kuhusu via vya uzazi vya mwanamke vinavyofanya kazi.
Kongamano likiendelea.
Mwanafunzi Juma Nasoro kutoka Sekondari ya Mabibo akitoa mada kuhusu via vya uzazi vya mwanaume vinavyofanya kazi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...