Rais anakubalika zaidi miongoni mwa makundi ya wazee na wenye kiwango kidogo cha elimu

15 Juni 2017, Dar es Salaam: Asilimia 71 ya wananchi wanaukubali utendaji wa Rais Magufuli tangu alipoingia madarakani. Kiwango hiki kimeshuka kutoka asilimia 96 mwezi Juni 2016.  Viwango vya kukubalika kwa Rais vinatofautiana katika makundi mbalimbali:
  • Asilimia 68 wenye umri chini ya miaka 30 wanamkubali Rais ikilinganishwa na asilimia 82 wenye umri zaidi ya miaka 50
  • Asilimia 75 ya wananchi wenye elimu ya msingi au chini yake wanamkubali Rais ikilinganishwa na asilimia 63 ya wale wenye elimu ya sekondari au zaidi
  • Asilimia 75 ya wananchi masikini wanamkubali Rais ikilinganishwa na asilimia 66 ya wananchi matajiri.
Viwango vya kukubalika kwa viongozi wengine navyo pia vimeshuka katika kipindi hicho hicho.
  • Wabunge:  Kukubalika kwa utendaji wa wabunge kumeshuka kutoka asilimia 79 (Juni 2016) hadi asilimia 58 (Aprili 2017).
  • Madiwani: Kukubalika kwa utendaji wa madiwani kumeshuka kutoka asilimia 74 (Juni 2016) hadi asilimia 59 (Aprili 2017).
  • Wenyeviti wa vijiji/mitaa: Kukubalika kwa utendaji wa wenyeviti wa vijiji/mitaa kumeshuka kutoka asilimia 78 (Juni 2016) hadi asilimia 66 (Aprili 2017).
  • -----------------------------------------------------------
    15 June 2017, Dar es Salaam: 
    Seven out of citizens (71%) approve of the performance of President Magufuli since taking office. This is down from 96% in June 2016. Approval ratings for the President vary between groups.
    • 68% of those under age 30 approve of the President compared to 82% of those over 50
    • 75% of citizens with no education or some primary approve of the President compared to 63% of those with secondary education or higher
    • And approval is slightly higher among poorer citizens (75%) than among the richest (66%).
    Approval ratings for other political leaders have also fallen over the same period.
    • MPs: 58% approval rating (April 2017) compared to 68% (June 2016)
    • Councilors: 59% approval rating (April 2017) compared to 74% (June 2016)
    • Village / street chair-people: 66% approval rating (April 2017) compared to 78% (June 2016)
  • KUPATA TAARIFA KAMILI BOFYA HAPA/FOR MORE CLICK HERE

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...