Na.Vero Ignatus Kilimanjaro.
Wito umetolewa kwa waongoza watalii nchini kutoa
ushirikiano ,kuwapendekeza watakaoingia katika kinyang'anyiro cha
kumtafuta mshindi wa Tuzo ambayo imeandaliwa kwaajili ya kumpata
Balozi atakaewawakilisha waongoza utalii nchini Tanzania,Afrika ya
Mashariki na Kati .
Akizungumza na blog hii Muasisi na mwenyekiti wa Tuzo
hiyo Sadock Mugetta amesema kuwa tuzo inafahamika
kama TANZANIA TOUR GUIDE AWARDS ambapo
mwaka jana ilikuwa imegawanyika katika vipengele vya
kumtafuta muongoza watalii bora wa Mlima,Safari pamoja na Wapagazi,ila
mwaka huu wameongeza vipengele viwili ambavyo ni Muongoza utalii wa
Utamaduni pamoja na Mpishi bora.
Sadock amesema kuwa wameamua kuwepo kwa Tuzo hiyo
kutokana hali halisi iliyopo ya ugumu wa kazi wanayoifanya waongoza
watalii (Mabalozi) ili mshindi atakayepatikana atawawakilisha
katika mambo yao ambayo wanataka Serikali iyafahamu,pamoja na wageni
mbalimbali waitambue Tanzania pamoja na vivutio vya Utalii
vilivyopo.
Ameongeza kuwa tangia kuanzishwa kwa huduma
ya utalii hapa nchini waongoza Watalii hawajawahi kupewa
kipaumbele, hivyo ni vyema Serikali ikatambua kuwa muongozaji watalii
huwa anatumumia 99% ya muda wao kukaa na mgeni awapo
nchini na anapewa taarifa zote sahihi na muhimu hadi anaondoka
nchini.
Wa kwanza kushoto ni Muasisi wa Tanzania Tour Guide Awards Sadock Mugetta, aliyepo kushot kwake ni Katibu wa Freelance Guides Society of Tanzania(FGST )anayefuata ni mjumbe wa wakiwa katika maonyesho ya (3)Utalii ya Kilifair katika uwanja wa Chuo cha Ushirika Moshi Mkoani Kilimanjaro.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...