Na Mathew Kwembe, Mtwara

Waganga wafawidhi wa vituo vya afya, na Waratibu elimu kata kutoka Halmashauri 93 zilizo katika mikoa 13 nchini inayotekeleza Mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3) nchini wameanza mafunzo ya siku mbili juu ya namna ya kutumia mfumo mpya wa uhasibu na utoaji taarifa za fedha unaojulikana kwa Kiingereza kama Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS).

Kwa mujibu wa Mkuu wa Kitengo cha Tehama na Mawasiliano kutoka Mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3) bwana Desderi Wengaa, mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo watoa huduma katika vituo vya kutolea huduma na kusaidia upatikanaji wa taarifa sahihi katika mahesabu ya mapato na matumizi ya halmashauri.

Bwana Wengaa alisema kuwa kuunda kwa mfumo huo kutasaidia kuhakikisha fedha za ruzuku zinasimamiwa vizuri na taarifa za matumizi yake zinatolewa kwa usahihi tofauti na ilivyokuwa mwanzo.Alisema kuwa FFARS itawapatia watoa huduma mfumo sanifu uliorahisishwa ambao utawawezesha kutunza taarifa za fedha zinazotolewa na zilizopo katika vituo vyao. 

Bwana Wengaa aliongeza kuwa FFARS itaweza kufuatilia matumizi ya fedha hizo katika kufikia malengo ya utoaji huduma na kuhakikisha yanaendana na sheria za manunuzi na utoaji taarifa. “Taarifa hizi zitasaidia Serikali kuimarisha Mfumo wa Usimamizi wa Fedha za Umma na kuongeza uwazi, na hivyo watoa huduma wa afya kuwa na wajibu kwa jamii wanayoihudumia,” alisema.
Mkuu wa Kitengo cha Tehama na Mawasiliano kutoka Mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3) bwana Desderi Wengaa akizungumza na waratibu elimu kata na waganga wafawidhi wa vituo vya afya kutoka Manispaa ya Mtwara Mikindani na Mtwara DC (hawapo pichani) kuhusu malengo ya kuanzishwa kwa mfumo mpya wa uhasibu na utoaji taarifa za fedha unaojulikana kwa Kiingereza kama Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS).
Baadhi ya Waganga wafawidhi wa vituo vya afya kutoka Manispaa ya Mtwara Mikindani na Mtwara DC wakimsikiliza Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Mtwara Mikindani Mhandisi Sambwe Sijabaje (hayupo pichani) wakati alipofungua mafunzo ya siku mbili kuhusu namna ya kuutumia mfumo mpya wa uhasibu na utoaji taarifa za fedha unaojulikana kwa Kiingereza kama Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS).
Baadhi ya Waratibu wa Elimu Kata kutoka Manispaa ya Mtwara Mikindani na Mtwara DC wakimsikiliza Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Mtwara Mikindani Mhandisi Sambwe Sijabaje (hayupo pichani) wakati alipofungua mafunzo ya siku mbili kuhusu namna ya kuutumia mfumo mpya wa uhasibu na utoaji taarifa za fedha unaojulikana kwa Kiingereza kama Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...