Na Karama Kenyunko, Globu ya Jamii.

Kamishana wa usimamizi wa mipaka idara ya Uhamiaji Tanzania, Samwel Magweiga, amepiga marufuku Mawakala wanaojihusisha na shughuli za uhamiaji na kuwataka waache mara moja kufanya hivyo.

Badala yake amewataka wananchi wanaohitaji huduma hiyo kufika ofisi husika ya Uhamiaji.

Kamishana Magweiga ametoa wito huo leo, wakati akizungumzia ukamatwaji wa watu watano wenye umri wa kati ya miaka 55 na 64 ambao walikutwa wakimiliki ofisi na mitambo wa kughushi nyaraka mbalimbali ikiwamo ya kughushi miradi ya maendeleo ya Serikali na machine za risiti za kielektroniki (EFDs).
Kufuatia ukamataji huo, Kamishna Magweiga amewaomba wananchi kutoa ushirikiano kwa idara ya Uhamiaji ili kudhibiti mianya ya watu wanaojihusisha na kughushi nyaraka za aina mbalimbali kwa kuwa zinapelekea uhujumu wa uchumi.

Mapema wiki hii, makachero kutoka ofisi za uhamiaji baada ya kupata taarifa kutoka kwa wasalimia wema kuhusu kuwepo kwa hujuma hiyo, walifanya msako na kuwakamata wazee watano ambao ofisi yao ipo eneo la BibiTiti Mohammed kiwanja namba 16/47 lililopo Wilaya ya Ilala mtaa wa Mtendeni.

Wazee waliokamatwa ni Hemed Ali Mchepe(56), Edga Samson Mwafongo(55), Huruma Mwakidete(57), David Tumpange (64),At human Mohammed (61) na Simon Joseph Veso (62).


Amesema, “kuna magenge ya wahalifu huko mitaani ambao wanafanya kazi kwa niaba ya serikali, hawa ni wahujumu uchumi, ni lazima wafichuliwe.” Amesisitiza Kamishna Magweiga.


Ameongeza kuwa, nyaraka hizo za mara nyingi zimekuwa zinatumika kuchukua hati za kusafiria, mikopo benki na kupelekea benki husika kupata hasara na serikali kukosa mapato.

Amesema, upelelezi dhidi ya watuhumiwa hao umekamilika na siku yoyote watapelekwa mahakamani ila badoa wanahitaji kujua mtandao wao ni mkubwa kiasi gani na upo hapa nchini pekee ama na nje ya nchi.

Wakielezea jinsi walivyokamatwa mbele ya Kamishana mzee David Tumpange alikubali kuwa yeye ni mmiliki wa ofisi iliyokutwa na nyaraka hizo za kughushi iliyopo eneo la barabara ya Bibi Titi Mohammed na kwamba yeye hashughuliki nayo alimkabidhi ndugu yake Huruma Mwakidete.

Aliongeza kuwa, kwa sasa yeye anajishughulisha na masuala ya ujenzi na siku ya tukio, alikwenda kwenye ofisi yake hiyo kwa ajili ya kumsalimia ndugu yake huyo aliyemkabidhi ofisi na vyote vilivyokutwa humo havitambui.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...