Watanzania  wameshauriwa kuchangamkia fursa ya kutembelea  maeneo matakatifu nchini Israel kwa gharama nafuu inayokadiriwa kuwa kati ya nafuu inayokadiriwa kuwa kati ya Dola za Kimarekani 1700 na 1800. 
 Mkurugenzi Mtendaji Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Bibi Devota Mdachi,  amesema jijini jana kuwa wadau wa utalii wa Israel wangependa kuona Watanzania wanatembelea Israel. 


Bibi Mdachi akiongozana na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Aloyce Nzuki ambaye alikuwa kiongozi wa msafara,  walitembelea Israel kwa siku tatu, walikutana na na wadau wa sekta ya utalii na kuwaeleza  vivutio vilivyopo nchini.

“Tumetembelea maeneo mengi ya kiroho ikiwemo miji ya Nazareth na Jerusalem, wenyeji wetu wamenipa ujumbe kuwa wanahitaji Watanzania waende wakahiji katika maeneo hayo kwa bei nafuu inayokadiriwa kuwa kati ya Dola za Kimarekani 1700 na 1800. 
“Fursa hii ni nzuri tafadhali tusiiache kwa sababu mbali ya hija lakini kuna mambo mengi mengine.  Watakaokwenda watakutana na raia wa mataifa mengine watawauliza kuhusiana na Tanzania,  maana yake mtageuka mabalozi wetu na kuvutia watalii wengi zaidi,” alisema Bibi. Mdachi. 
Alibainisha kuwa kiasi hicho cha Dola 1700 au 1800 kinahusisha nauli ya kwenda na kurudi, malazi pamoja na ziara ya maeneo matakatifu ndani ya miji husika. 
“Kampuni ya Another World imeahidi ifikapo Agosti mwaka huu wataleta watalii kutoka Israel watakaotembelea maeneo ya Hifadhi ya Katavi, Mahale, Ngorongoro na Zanzibar. 
Mmiliki wa kampuni ya Another World, Bw Shlomo Carmel ameahidi kuleta watalii zaidi ya 2000 kati ya Agosti na Disemba mwaka huu.


Vilevile kuna wawekezaji katika sekta ya hoteli za viwango vya kimataifa wameahidi kuja kuwekeza nchini, kifupi imekuwa ni ziara yenye tija kwetu sote,” alibainisha Bibi. Mdachi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...