Naibu Mwanasheria wa Serikali Bw. Gerson Mdemu akisisitiza jambo wakati wa mkutano wake wa kazi na watumishi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Tabora wakati wa wiki ya Utumishi wa Umma. Katika Mkutano huo Naibu Mwanasheria Mkuu, amesisitiza watumishi wa Ofisi yake kuzingatia misingi na maadili ya Utumishi. Kushoto kwa Naibu Mwanasheria Mkuu ni Wakili wa Serikali Mfawidhi Bw. Jackson Bulashi na kulia ni Bw. Benny Kabungo Mkurugenzi wa Utumishi na Raslimali Watu.
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Tabora wakimsikiliza Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali wakati wa kikao kazi ikiwa ni sehemu ya maadhimisho wa wiki ya Utumishi wa Umma. Katika kuadhimisha wiki ya Utumishi wa Umma Ofisi ya Mwanasheria Mkuu ( 16-23) ilitenga siku mbili za kukutana na wadau na watumishi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...