NA HAMZA TEMBA - WMU
Waziri
wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe kwa kushirikiana na Balozi wa
Ujerumani hapa nchini, Egon Konchanke amezindua Mradi wa Uhifadhi na Maendeleo
ya Ikolojia ya Pori la Akiba la Selous SECAD (Selous Ecosytem Conservation and
Development Program) ambao umefadhiliwa na Serikali ya Ujerumani kwa
ushirikiano na Serikali ya Tanzania, mradi huo utatekelezwa na Wizara ya
Maliasili na Utalii kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania TAWA,
WWF (World Wildlife Fund) na FZS (Frankfurt Zoological Society).
Akizungumza
katika hafla iliyofanyika jana, Matambwe na Tagalala Selous, Mkoani Morogoro, Waziri
Maghembe alisema Serikali ya Ujerumani kupitia benki ya KFW imechangia
Euro Mil. 18 (sawa na Shilingi Bil. 45.124) katika mradi huo wa miaka
mitano huku mashirika ya WWF (World Wildlife Fund) na FZS (Frankfurt Zoological
Society) yakichangia Euro laki 4 kila moja (sawa na Shilingi bil. 2.005) katika mradi huo.
Pamoja na uzinduzi huo alizindua pia Mpango Kazi wa Dharura wa kuendeleza pori
hilo.
"Mradi
huu ni muhimu sana kwakua utasaidia kuongeza nguvu kwenye jitihada zetu za
kuendeleza na kuimarisha hifadhi ya pori hili la Selous ikiwemo upatikanaji wa
vitendea kazi muhimu pamoja na kutuongezea nguvu kwenye mapambano dhidi ya
ujangili", alisema Prof. Maghembe.
Alisema
jitihada ambazo Serikali imeshazifanya katika pori hilo ni pamoja na kuimarisha
doria za ndege zenye rubani na zisizo na rubani (drones), kutoa mafunzo ya
jeshi usu kwa askari, kuongeza maaskari pamoja na vitendea kazi ambapo katika
mwaka ujao wa fedha Serikali itatoa magari mengine 15 kusaidia pori hilo.
"Pamoja
na jitihada hizo tunawekeza dola za kimarekani Milioni 156 (sawa na Shilingi
bilioni 349.441) kwa ajili ya kuboresha pori hili (Selous), Ruaha, Mikumi, Rungwa
na Kitulo kuhakikisha watalii wanatembelea maeneo haya na kuondoa kile kikwazo
cha wao kutotembelea hifadhi za kusini, hiyo inaenda sambamba na kuimarishwa
kwa shirika la ndege la Serikali la Air Tanzania na kuondoa changamoto
iliyokuwepo ya usafiri wa anga", alisema Prof. Maghembe.
Waziri
wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (kulia) akizindua Mradi
wa Uhifadhi na Maendeleo wa Ikolojia ya Pori la Akiba la Selous (SECAD)
ambao umefadhiliwa na Serikali ya Ujerumani kwa ushirikiano na Serikali
ya Tanzania katika hafla iliyofanyika jana Matambwe, Selous Mkoani
Morogoro. Wanaoshudia kulia kwake ni Balozi wa Ujerumani, Egon
Konchanke, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili, Meja Jenerali Gaudence
Milanzi na Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais, Prof. Faustin Kamuzora.
Waziri
wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (kulia) akimkabidhi
Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori wa Wizara hiyo, Prof. Alexander
Songorwa Mpango Kazi wa Dharura wa Kuendeleza Pori la Akiba la Selous
baada ya kuuzindua sambamba na mradi wa Uhifadhi na Maendeleo ya
Ikolojia ya Pori la Akiba la Selous (SECAD). Kulia kwake ni Balozi wa
Ujerumani, Egon Konchanke, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali
Gaudence Milanzi, Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais, Prof. Faustin
Kamuzora, Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori
Tanzania, Martin Loibooki na Muwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa TANAPA,
Dkt. Dembe.
Waziri
wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (kushoto) na Balozi wa
Ujerumani hapa nchini, Egon Konchanke wakikata utepe kuashiria uzinduzi
wa magari sita aina ya Land Cruiser ambayo ni sehemu ya Mradi
aliouzindua wa Uhifadhi na Maendeleo ya Ikolojia ya Pori la Akiba la
Selous (SECAD).
Magari sita aina ya Land Cruiser yaliyotolewa na Serikali ya Ujerumani kama sehemu ya mradi wa SECAD.
Waziri
wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Mghembe (kushoto) akipokea zawadi
ya picha yenye ujumbe wa Mashujaa wa Kuokoa Selous kutoka kwa
Mkurugenzi wa Afrika wa WWF Ujerumani, Philipp Goltenboth (kulia).
Anaeshuhudia katikati ni Mkurugenzi Mkaazi wa WWF Tanzania, Dkt. Amani
Ngusaru.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...