NA HAMZA TEMBA - WMU

Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe kwa kushirikiana na Balozi wa Ujerumani hapa nchini, Egon Konchanke amezindua Mradi wa Uhifadhi na Maendeleo ya Ikolojia ya Pori la Akiba la Selous SECAD (Selous Ecosytem Conservation and Development Program) ambao umefadhiliwa na Serikali ya Ujerumani kwa ushirikiano na Serikali ya Tanzania, mradi huo utatekelezwa na Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania TAWA, WWF (World Wildlife Fund) na FZS (Frankfurt Zoological Society).

Akizungumza katika hafla iliyofanyika jana, Matambwe na Tagalala Selous, Mkoani Morogoro, Waziri Maghembe alisema Serikali ya Ujerumani kupitia benki ya KFW imechangia Euro Mil. 18 (sawa na Shilingi Bil. 45.124) katika mradi huo wa miaka mitano huku mashirika ya WWF (World Wildlife Fund) na FZS (Frankfurt Zoological Society) yakichangia Euro laki 4 kila moja (sawa na Shilingi bil. 2.005) katika mradi huo. Pamoja na uzinduzi huo alizindua pia Mpango Kazi wa Dharura wa kuendeleza pori hilo.

"Mradi huu ni muhimu sana kwakua utasaidia kuongeza nguvu kwenye jitihada zetu za kuendeleza na kuimarisha hifadhi ya pori hili la Selous ikiwemo upatikanaji wa vitendea kazi muhimu pamoja na kutuongezea nguvu kwenye mapambano dhidi ya ujangili", alisema Prof. Maghembe.

Alisema jitihada ambazo Serikali imeshazifanya katika pori hilo ni pamoja na kuimarisha doria za ndege zenye rubani na zisizo na rubani (drones), kutoa mafunzo ya jeshi usu kwa askari, kuongeza maaskari pamoja na vitendea kazi ambapo katika mwaka ujao wa fedha Serikali itatoa magari mengine 15 kusaidia pori hilo.

"Pamoja na jitihada hizo tunawekeza dola za kimarekani Milioni 156 (sawa na Shilingi bilioni 349.441) kwa ajili ya kuboresha pori hili (Selous), Ruaha, Mikumi, Rungwa na Kitulo kuhakikisha watalii wanatembelea maeneo haya na kuondoa kile kikwazo cha wao kutotembelea hifadhi za kusini, hiyo inaenda sambamba na kuimarishwa kwa shirika la ndege la Serikali la Air Tanzania na kuondoa changamoto iliyokuwepo ya usafiri wa anga", alisema Prof. Maghembe. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (kulia) akizindua Mradi wa Uhifadhi na Maendeleo wa Ikolojia ya Pori la Akiba la Selous (SECAD) ambao umefadhiliwa na Serikali ya Ujerumani kwa ushirikiano na Serikali ya Tanzania katika hafla iliyofanyika jana Matambwe, Selous Mkoani Morogoro. Wanaoshudia kulia kwake ni Balozi wa Ujerumani, Egon Konchanke, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili, Meja Jenerali Gaudence Milanzi na Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais, Prof. Faustin Kamuzora.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (kulia) akimkabidhi Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori wa Wizara hiyo, Prof. Alexander Songorwa Mpango Kazi wa Dharura wa Kuendeleza Pori la Akiba la Selous baada ya kuuzindua sambamba na mradi wa Uhifadhi na Maendeleo ya Ikolojia ya Pori la Akiba la Selous (SECAD). Kulia kwake ni Balozi wa Ujerumani, Egon Konchanke, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Gaudence Milanzi, Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais, Prof. Faustin Kamuzora, Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania, Martin Loibooki na Muwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa TANAPA, Dkt. Dembe. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (kushoto) na  Balozi wa Ujerumani hapa nchini, Egon Konchanke wakikata utepe kuashiria uzinduzi wa magari sita aina ya Land Cruiser ambayo ni sehemu ya Mradi aliouzindua wa Uhifadhi na Maendeleo ya Ikolojia ya Pori la Akiba la Selous (SECAD).
 Magari sita aina ya Land Cruiser yaliyotolewa na Serikali ya Ujerumani kama sehemu ya mradi wa SECAD.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Mghembe (kushoto) akipokea zawadi ya picha yenye ujumbe wa Mashujaa wa Kuokoa Selous kutoka kwa Mkurugenzi wa Afrika wa WWF Ujerumani, Philipp Goltenboth (kulia). Anaeshuhudia katikati ni Mkurugenzi Mkaazi wa WWF Tanzania, Dkt. Amani Ngusaru.
Taswira mwanana ya baadhi ya Twiga ndani ya Pori la Akiba la Selous.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...