Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu(sera, bunge, kazi, vijana, na watu wenye ulemavu), Mhe Jenista Mhagama, akiwa na Naibu Waziri Mhe Anthony Mavunde wakikagua karakana na baadhi ya kazi zinazofanywa na Taasisi ya Don Bosco wanaotekeleza mradi wa Programu ya kitaifa ya kukuza ujuzi wa nguvu kazi wa stadi za maisha ya Taifa kwa vijana, Mkoani Iringa mpango ambao utawanufaisha vijana elfu tatu mianne 3,400 mpango unaogharamiwa na Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Mhe, Dkt. John Pombe Magufuli.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu(sera, bunge, kazi, vijana, na watu wenye ulemavu), Mhe Jenista Mhagama amezindua Programu ya kitaifa ya kukuza ujuzi wa nguvu kazi wa stadi za maisha ya Taifa kwa vijana, Mkoani Iringa mpango ambao utawanufaisha vijana elfu tatu mianne 3,400 mpango  unaogharamiwa na Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Mhe, Dkt. John Pombe Magufuli.

Mhe Mhagama amesema mpango huu ni sehemu ya kuwaandaa vijana ambao watashiriki katika mapinduzi ya viwanda nchi Tanzania na utasaidia kutoa fursa kwa vijana kujiajiri na kuajiriwa kupitia mafunzo ya Uanagenzi, katika nyanja za ujenzi, tehama, ufundi magari, na ushonaji nguo katika mikoa yote nchini Tanzania.

Katika awamu hii ya kwanza, mpango huu unaendeshwa kwa pamoja baina ya Serikali ya Tanzania na taasisi ya Wasalesiani wa Don Bosco Tanzania.

Uzinduzi huo umeshuhudiwa na Naibu waziri Mhe Anthony Mavunde, Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe Amina Masenza, Wabunge kutoka mkoa wa Iringa, na Njombe na Mkuu wa Shirika la Wasalesiani wa Don Bosco Africa Mashariki Fr. Simon Asira.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu(sera, bunge, kazi, vijana, na watu wenye ulemavu), Mhe Jenista Mhagama akiangalia baadhi ya bidhaa katika moja ya mabanda baada ya kuzindua Programu ya kitaifa ya kukuza ujuzi wa nguvu kazi wa stadi za maisha ya Taifa kwa vijana, Mkoani Iringa. Kulia ni Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. Anthony Mavunde.
Picha ya Pamoja.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...