Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo ndg John Lipesi Kayombo akiwa ameambatana na timu ya wakuu wa idara wa Manispaa ya Ubungo, walitembelea na kujionea maandalizi ya Nanenane katika eneo la Itungi Mkoani Morogoro.

Akiwa katika eneo hilo la Manispaa ya Ubungo, maalum kwa maonesho ya Nanenane,Mkurugenzi na timu yake wamejionea aina mbalimbali za mazao ambayo tayari yamepandwa zikiwemo mboga mboga za kila aina.

Pia Manispaa tayari imetengeneza bwawa la kisasa la samaki aina ya Tilapia, na banda la kisasa la ufugaji ng'ombe ,

Baada ya kuona maandalizi hayo Mkurugenzi ameipongeza idara ya kilimo kwa maandalizi hayo na kuahidi kutoa ushirikiano kwa kuwezesha pale patakapohitaji uwezeshwaji yuko tayari, ili kuhakikisha maonyesho hayo yanafana na kuwa ya tofauti licha ya Ubungo kuwa ni Halmashauri mpya .

Naye kaimu mkuu wa idara ya kilimo na mifugo ,Salimu Msuya amesema wao kama idara wamejipanga vizuri na wanaamini watafanya vizuri katika maonyesho hayo,hivyo wanawakaribisha wananchi wote kutembelea banda la Ubungo siku hiyo ya Nanenane.

Tarehe 8/8/ kila mwaka Tanzania huadhimisha sikukuu ya wakulima.

*Ubungo mpya, Ubungo ya tofauti *

 Mkurugenzi John Kayombo na Timu ya Wakuu wa  Idara wakikagua Ujenzi wa  Bwawa la samaki
 Afisa Kilimo Salim Msuya akitoa Maelekezo kwa timu ya Wakuu was Idara Kuhusu Kilimo cha Mbogamboga kilichofanyika eneo hilo
Mkurugenzi wa  Manispaa ya Ubungo John Kayombo na Wakuu was Idara Wakipata Maelekezo Kutoka ka Afisa wa Kilimo ndugu Salim Msuya

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...