NA HAMZA TEMBA - WMU

Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Bodi ya Utalii Tanzania TTB, imefanya semina ya mafunzo ya siku moja kwa wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) kwa lengo la kuwajengea uelewa wajumbe hao kuhusu majukumu ya taasisi hiyo ambayo imefanyika jana mjini Dodoma na kuhudhuriwa na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhandisi Ramo Makani na Katibu Mkuu, Meja Jenerali Gaudence Milanzi.

Akizungumza katika semina hiyo, Meneja wa Huduma za Utalii wa taasisi hiyo, Philip Chitaunga alisema bodi hiyo iliyoanzishwa mwaka 1993 ilipewa jukumu la jumla la kukuza sekta ya utalii nchini ikiwemo kutumia mbinu mbalimbali za utangazaji, kuhamasisha uendelezaji wa mazao ya utalii na miundombinu yake, kufanya tafiti za masoko na utalii kwa ujumla pamoja na kuhamasisha uelewa wa watanzania kufahamu umuhimu na faida za utalii.

Alisema taasisi hiyo imefanya juhudi mbalimbali za kutangaza utalii wa Tanzania nje ya nchi ikiwemo kuratibu ziara za waandishi wa habari za kitalii, kuweka matangazo katika magazeti ya utalii ya kimataifa, kushiriki katika maonesho ya utalii ya kimataifa na kutangaza kupitia Televisheni za kimataifa kama CNN ya Marekani.

“Jitihada zingine tulizofanya ni kutumia balozi zetu nje ya nchi na mabalozi wa utalii wa hiari yaani 'Goodwill Ambasadors', kutumia mitandao ya kijamii na matangazo kwenye vyombo vya usafiri vya umma ambapo mwaka 2008 hadi 2009 tulitangaza kwenye mabasi 124 jijini london Uingereza, taxi 100, treni mbalimbali na katika uwanja wa ndege wa Heathrow” alisema Chitaunga.

Alisema jitihada za hivi karibuni za kutangaza utalii zimefanyika kupitia michezo ya Ligi Kuu ya Uingereza ikiwemo timu za mpira wa miguu za Seattle Sounders na Sunderland, kupitia majarida, CD na filamu fupi kwa lugha mbalimbali kama Kiingereza, Kijerumani, Kifaransa na Kiswahili. Pia, kupitia tovuti maalum ya utalii ya taifa (www.tanzaniatourism.gotz), App kwenye ‘Smart Phones’ na kufanya ziara za utangazaji wa utalii yaani Roadshows katika nchi za China, Afrika ya Kusini, bara la Ulaya, Amerika na Australia.
Naibu Waziri wa Maliasili, Mhandisi Ramo Makani (kushoto) akizungumza jana mjini Dodoma katika semina iliyoandaliwa na Wizara hiyo kupitia Bodi ya Utalii Tanzania kwa ajili ya kuwajengea uelewa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) kuhusu majukumu ya bodi hiyo. Kulia ni Mwenyekiti wa kamati hiyo, Albert Obama. 
Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja Jenerali Gaudence Milanzi (kushoto) akizungumza jana mjini Dodoma katika semina iliyoandaliwa na Wizara hiyo kupitia Bodi ya Utalii Tanzania kwa ajili ya kuwajengea uelewa wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) kuhusu majukumu ya bodi hiyo. Katikati ni Naibu Waziri wa Maliasili, Mhandisi Ramo Makani na Mwenyekiti wa kamati hiyo, Albert Obama.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC), Albert Obama (kulia) akizungumza jana mjini Dodoma katika semina iliyoandaliwa na Wizara ya Maliasili kupitia Bodi ya Utalii Tanzania kwa ajili ya kuwajengea uelewa wajumbe wa kamati hiyo kuhusu majukumu ya bodi hiyo. Katikati ni Naibu Waziri wa Maliasili, Mhandisi Ramo Makani na Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja Jenerali Gaudence Milanzi. 
Meneja wa Huduma za Utalii wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Philip Chitaunga (kushoto) akiwasilisha mada ya jumla kuhusu shughuli za taasisi hiyo kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) katika semina iliyoandaliwa na Wizara hiyo kupitia bodi hiyo mjini Dodoma jana. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...