Honorius Mpangala

Moja ya misemo ya kiswahili inayopendwa kutumuwa na watanzania ni "usijisifie una mbio bali msifie na anayekukimbiza" msemo huu ungekuwa bora sana kuwa elezea klabu ya Simba kuwa walikua vyema msimu tofauti na msimu uliopita.

Msimu wa 2016/17 kwa upande wa klabu ya Yanga unaweza kusema ulikua mgumu sana na huenda ungewanyima taji kama tu wasingechukua maamuzi magumu baada ya kuona watu wanapangwa katika kikosi kwa mazoea,binafsi naamini taji la Yanga ni kwa marekebisho makubwa yaliyofanyika na Kocha George Lwandamina.

Tathimini yangu kwa msimu mzima kwa klabu ya Yanga.

Moja ilianza ligi ilikuwa na mchoko wa hali ya juu baada ya kuumaliza mwaka mzima wa kalenda wa 2016 kwa kufululiza kucheza mechi ikiwa ni kitu ambacho haikuzoeleka kwa wachezaji wake.

Mbili kiburi cha kujiona wakimataifa  kulisababisha Yanga iweza kuona michezo kama dhidi ya Stands Utd, Ndanda, Mbeya City kuwa migumu kwao tofauti na ilivyokua msimu uliopita.

Tatu,klabu ya yanga kukumbwa na changamoto ya mishahara ilikua ni moja ya sababu iliyowafanya wachezaji kukutwa na visununu kama Yale yaliyotokea kwa Vincent bossou aliyekuja kutofautiana na uongozi kwasababu ya malipo ya mshahara wake kama ilivyokua kwa Obrey Chirwa.

Majeruhi ya key player kama Juma Abdul, Donald Ngoma,Thaban Kamusoko, Amis Tambwe kwa nyakati tofauti watu waliochukua nafasi zao hawakuweza kuwa fit na kuisaidia klabu kucheza kwa kasi na kiwango kama cha waliopata majeruhi.
Nne, Matatizo ya Mwenyekiti wa klabu kulimfanya kukaa mbali na kushindwa kuwa karibu na wachezaji ambao waliamini uwepo wake katika kuwasapoti kulitoa hamasa kubwa kwao.

Tano, kuna haja kubwa ya kuandaa mikakati ya kuweza kufanikiwa katika michezo ya kimataifa kwani japo msimu uliopita timu iliishia hatua ya robo fainali ila mapungufu yalikuwa mengi kwasababu ya maandalizi ya klabu katika kuwakabili wapinzani wao.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...