Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro akizungumza na mkuu wa chuo cha ulinzi cha Taifa cha Rwanda Kamishina wa Polisi wa Rwanda Felix Namhoranye ofisini kwake makao makuu ya Jeshi la Polisi. Kamishina Namhoranye ni kiongozi wa msafara wa maafisa mbalimbali kutoka chuo cha ulinzi cha Taifa cha Rwanda ambao wapo nchini kwa ziara ya mafunzo. Picha na Hassan Mndeme – Jeshi la Polisi.

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro akizungumza na maofisa wa polisi kutoka nchi mbalimbali za Afrika mashariki na Afrika magharibi ambapo wanasoma chuo cha ulinzi cha Taifa cha Rwanda hawapo picha. Kushoto ni mkuu wa chuo cha ulinzi cha Taifa cha Rwanda, Kamishina Felix Namhoranye na kulia ni Kamishina wa Polisi Jamii , Mussa Alli Mussa – picha na Hassan Mndeme – Jeshi la Polisi.

Baadhi ya maafisa wa Polisi kutoka nchi mbalimbali za afrika mashariki na magharibi wanaosoma chuo cha ulinzi wa taifa cha Rwanda wakimsikiliza Mkuu wa Jeshi la Polisi wa Tanzania makao makuu ya Jeshi la ( hayupo picha ) wakati wa ziara yao ya mafunzo hapa nchini. Picha na Hassan Mndeme – Jeshi la Polisi.

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro akiwa katika picha ya pamoja na maafisa wa Polisi kutoka nchi mbalimbali wanaosoma chuo cha ulinzi wa taifa cha Rwanda. Ujumbe huo unaohusisha maofisa wa Polisi kutoka nchi za Afarika mashariki na Afrika magharibi unaongozwa na Kamishina wa Polisi wa Rwanda Felix Namhoranye ambaye ndiye mkuu wa chuo cha ulinzi cha ulinzi cha Rwanda wapo nchini Tanzania kwa ziara ya kijifunza namna taasisi mbalimbali zinavyoendeshwa hapa Tanzania. Picha Hassan Mndeme – Jeshi la Polisi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...