Mwanamuziki
wa Kimataifa kutoka nchini Congo, Ferre Gola, (wa pili kulia)
Mkurugenzi wa Kampuni ya Montage Ltd, Teddy Mapunda (kulia) na Mwalimu
Mkuu wa Shule ya Msingi Uhuru mchanganyiko, Anna Mshana, kwa pamoja
wakipaka rangi katika ukuta wa chumba cha darasa la Shule ya Msingi
Uhuru Mchanganyiko, wakati walipofika shuleni hapo kwa ajili ya kujionea
mazingira ya shule hiyo, baada ya kuomba kusaidiwa mahitaji hayo,
ambapo msaada huo umetokana na mauzo ya meza za Onyesho maalumu la
mwanamuziki huyo linalofanyika leo Alhamisi kwenye Hoteli ya Serena
jijini Dar es Salaam. Picha Zote na Muhidin Sufiani (MAFOTO)
Mwanamuziki
wa Kimataifa kutoka nchini Congo, Ferre Gola, (kushoto) na Christian
Bella, kwa pamoja wakipaka rangi katika ukuta wa chumba cha darasa la
Shule ya Msingi Uhuru Mchanganyiko, wakati walipofika shuleni hapo kwa
ajili ya kujionea mazingira ya shule hiyo, baada ya kuomba kusaidiwa
mahitaji hayo, ambapo msaada huo umetokana na mauzo ya meza za Onyesho
maalumu la mwanamuziki huyo linalofanyika leo Alhamisi kwenye Hoteli ya
Serena jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi
wa Kampuni ya Montage Ltd, Teddy Mapunda, akizungumza na waandishi wa
habari wakati wa ziara ya mwanamuziki wa kimataifa kutoka Congo, Ferre
Gola (wa pili kulia) na Christian Bella (kulia) walipofika SHule ya
Uhuru Mchanganyiko kwa ajili ya kukabidhi na kupaka rangi katika baadhi
ya vyumba vya madarasa ya shule hiyo. msaada huo umetokana na mauzo ya
meza za Onyesho maalumu la mwanamuziki huyo linalofanyika leo Alhamisi
kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Mwalimu
Mkuu wa Shule ya Msingi Uhuru Mchanganyiko, Anna Mshana, akizungumza na
waandishi wa habari wakati wa ziara ya mwanamuziki wa kimataifa kutoka
Congo, Ferre Gola (wa pili kulia) na Christian Bella (kulia) walipofika
Shule ya Uhuru Mchanganyiko kwa ajili ya kukabidhi na kupaka rangi
katika baadhi ya vyumba vya madarasa ya shule hiyo. msaada huo umetokana
na mauzo ya meza za Onyesho maalumu la mwanamuziki huyo linalofanyika
leo Alhamisi kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...