Mwanamuziki wa Kimataifa kutoka nchini Congo, Ferre Gola, (wa pili kulia) Mkurugenzi wa Kampuni ya Montage Ltd, Teddy Mapunda (kulia) na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Uhuru mchanganyiko, Anna Mshana, kwa pamoja wakipaka rangi katika ukuta wa chumba cha darasa la Shule ya Msingi Uhuru Mchanganyiko, wakati walipofika shuleni hapo kwa ajili ya kujionea mazingira ya shule hiyo, baada ya kuomba kusaidiwa mahitaji hayo, ambapo msaada huo umetokana na mauzo ya meza za Onyesho maalumu la mwanamuziki huyo linalofanyika leo Alhamisi kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam. Picha Zote na Muhidin Sufiani (MAFOTO)
 Mwanamuziki wa Kimataifa kutoka nchini Congo, Ferre Gola, (kushoto) na Christian Bella,  kwa pamoja wakipaka rangi katika ukuta wa chumba cha darasa la Shule ya Msingi Uhuru Mchanganyiko, wakati walipofika shuleni hapo kwa ajili ya kujionea mazingira ya shule hiyo, baada ya kuomba kusaidiwa mahitaji hayo, ambapo msaada huo umetokana na mauzo ya meza za Onyesho maalumu la mwanamuziki huyo linalofanyika leo Alhamisi kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam. 
 Mkurugenzi wa Kampuni ya Montage Ltd, Teddy Mapunda, akizungumza na waandishi wa habari wakati wa ziara ya mwanamuziki wa kimataifa kutoka Congo, Ferre Gola (wa pili kulia) na Christian Bella (kulia) walipofika SHule ya Uhuru Mchanganyiko kwa ajili ya kukabidhi na kupaka rangi katika baadhi ya vyumba vya madarasa ya shule hiyo. msaada huo umetokana na mauzo ya meza za Onyesho maalumu la mwanamuziki huyo linalofanyika leo Alhamisi kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
 Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Uhuru Mchanganyiko, Anna Mshana, akizungumza na waandishi wa habari wakati wa ziara ya mwanamuziki wa kimataifa kutoka Congo, Ferre Gola (wa pili kulia) na Christian Bella (kulia) walipofika Shule ya Uhuru Mchanganyiko kwa ajili ya kukabidhi na kupaka rangi katika baadhi ya vyumba vya madarasa ya shule hiyo. msaada huo umetokana na mauzo ya meza za Onyesho maalumu la mwanamuziki huyo linalofanyika leo Alhamisi kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...