Afya ya mtoto Mwenge aliyenusurika kifo baada ya kutumbukizwa chooni na kukaa humo kwa zaidi ya saa 14 kabla ya kuokolewa akiwa hai, inaendelea kuimarika huku akiendelea kupatiwa matibabu katika hospitali ya Kiomboi Wilayani Iramba.

Mtoto Mwenge alitupwa chooni na mama yake mzazi Winfrida Lori (23) mwanafunzi katika Chuo cha Uuguzi cha Kiomboi Wilayani Iramba ambapo mama huyo amekiri kujifungua mtoto huyo wa kiume katika Kijiji cha Luono Julai 3, saa mbili usiku kisha kumfunga vitambaa mdomoni na kumtumbukiza chooni.

Muuguzi Mkuu wa Hospitali ya Kiomboi Regina Alex amesema afya ya Mtoto Mwenge inaendelea kuimarika pamoja na hali ya mama mzazi wa mtoto huyo pia inaimarika tofauti na hapo awali ambapo alikuwa dhaifu na kushindwa kumnyonyesha mtoto.

“Winifrida alikuwa hawezi kumyonyesha mtoto Mwenge hapo mwanzoni lakini sasa hivi anamnyonyesha vizuri na maziwa yanatoka ya kutosha, Mtoto mwenge ana hali nzuri na sasa amefikisha uzito wa kilogramu 2.9 hali ambayo inaridhisha kwakweli”, ameeleza muuguzi huyo.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi (picha ya maktaba).


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...