Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Saimon Sirro, amefanya mabadiliko ya Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani pamoja na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya.
Katika
mabadiliko hayo, aliyekuwa Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama
Barabarani Naibu Kamishna wa Polisi Mohamed Mpinga anaenda kuwa Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Mbeya, na nafasi yake inachukuliwa na Kamishna
Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Fortunatus Musilimu.
Aidha, Aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya (DCP) Dhahiri Kidavashari amehamishiwa Makao Makuu ya Upelelezi.
Uhamisho
huo ni wa kawaida katika kuboresha utendaji wa kazi za Polisi kwa
mujibu wa kanuni, taratibu na miongozo ya Jeshi la Polisi.
Imetolewa na:
Barnabas D. Mwakalukwa – ACP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.
Makao Makuu ya Jeshi la Polisi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...