Kampuni ya Azam Media inazindua app za kisasa kwa ajili ya habari, michezo na matangazo ya televisheni. App hizo za aina yake katika mifumo ya Android na iOS, zinaanza kupatika leo Jumamosi kupitia Play Store ya Google na App Store ya Apple – unatakiwa kupakua app yenye rangi ya njano iliyoandikwa Azam Pay TV. 
Kupitia app hizo zilizosanifiwa kwa kuzingatia mahitaji ya wateja wa ndani na nje ya Tanzania zitakuwa na chaneli saba kwa kuanzia, ikitarajiwa chaneli nyingine zitaendelea kuongezwa.Chaneli hizo ni Azam One, Azam TWO, Sinema Zetu, Azam Sports HD, UTV, ZBC2 na Real Madrid.

CEO wa Azam Media, Tido Mhando, amesema app hizo zinatarajiwa kuleta mageuzi makubwa katika utoaji wa huduma za televesheni na kuendana na teknolojia ya kisasa katika soko. 
“Hatua hii tuliyofikia leo ni kielelezo tosha kuwa tunasikiliza wateja wetu wanataka nini na tunafanya jitihada kutoa huduma zilizo bora na zenye kukidhi viwango vinavyoendana na chapa Azam inayojulikana kote Afrika Mashariki kwa ubora,” ameeleza Mhando. 
Mhariri wa Masuala ya Mitandao wa Azam TV, Hassan Mhelela, amesema app hizo zimesanifiwa kuwa rahisi kuzitumia kwa kuzingatia umuhimu wa upatikanaji wa huduma za habari na televisheni kupitia vifaa vya mkononi. 
“Mfumo huu wa Azam TV app utawawezesha watu wengi zaidi kupata taarifa na kufuatilia vipindi vya kwenye televisheni kwa kutumia vifaa vya mkononi kama simu au tablet. Kinachotakiwa ni mtandao wenye nguvu unaokuwezesha kucheza video au kuangalia televisheni yaani streaming,” amesema Mhelela. 
Kwa kuanzia app hizo zinapatikana bure kwa yoyote mwenye kifaa chenye internet kinachotumia mfumo wa Android au iOS. 

Azam Media ni kampuni tanzu ya Bakhresa Group.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...