Na Robert Hokororo

Halmashauri ya wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga imepongezwa kwa hatua yake ya utekelezaji miradi mbalimbali ya maendeleo kwa ufanisi pamoja na changamoto za uhaba wa fedha.

Pongezi hizo zimetolewa leo na mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Boniphace Butondo wakati akifungua kikao cha Baraza la Madiwani kilichoketi kupokea taarifa za kata kwa kipindi cha robo ya nne ya mwaka.Butondo alisema miradi hiyo imetekelezwa kwa kiwango kizuri pamoja na changamoto ya uhaba wa fedha iliyoikabili halmashauri hiyo kwa kipindi hicho.

Alisema ushirikianoa baina ya madiwani na wataalamu kutoka halmashauri hiyo ndiyo siri ya mafanikio hayo ambayo ni tija kwa wananchi wanaowahudumia.Aidha, aliwapongeza wataalamu hao kutoka idara mbalimbali kwa kuwa na usimamizi mzuri ikiwemo wa fedha na maeneo ambayo miradi hiyo inatekelezwa na kuwataka waendelee kushikamana.
Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kishapu, Boniphace Butondo akizungumza wakati akifungua kikao cha Baraza la Madiwani la kupokea na kujadili tarifa za kata za robo ya nne ya mwaka. Wengine pichani kushoto ni Makamu mwenyekiti wa halmashauri, Edward Shigela na Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo, Stephen Magoiga.

Mkurugenzi mtendaji halmashauri ya wilaya ya Kishapu, Stephen Magoiga akizungumza wakati wa kikao hicho. Wengine pichani kuanzia kushoto ni Katibu Tawala Wilaya, Shadrack Kangese, Makamu mwenyekiti wa halmshauri, Edward Shigela na Mwenyekiti Boniphace Butondo.

Madiwani na wataalamu kutoka halmashauri hiyo wakifuatilia kikao hicho cha kupokea na kujadili tarifa za maendeleo ya kata.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...